Hadithi za Maandiko
Yesu Kristo Atakuja Tena—Ono la Yohana juu ya tumaini katika Yesu Kristo


Ufunuo

Yesu Kristo Atakuja Tena

Ono la Yohana juu ya tumaini katika Yesu Kristo

Yohana akiwa amesimama karibu na Yesu Kristo.

Mtume Yohana alikuwa na ono maalum. Alimwona Yesu Kristo, ambaye alimwonyesha Yohana mambo mengi kuhusu yaliyopita na yajayo. Alimwambia Yohana aandike mambo aliyoyaona. Yesu alijua Watakatifu walikuwa wakijaribu kwa uwezo wao wote kumfuata Yeye. Yesu aliwataka wawe na tumaini kwamba Yeye ana nguvu zaidi kuliko uovu ulimwenguni.

Ufunuo 1:1–2, 9–11, 13–15, 19; 2–3

Baba wa Mbinguni mkono Wake ukiwa kwenye bega la Yesu Kristo.

Katika ono lake, Yohana aliona kitabu ambacho hakuna mtu ambaye angeweza kukifungua. Kisha Yohana alimwona mwanakondoo aliyemwakilisha Yesu Kristo; Angeweza kukifungua kitabu hicho. Yohana alijifunza kwamba kabla dunia haijaumbwa, Baba wa Mbinguni alimchagua Yesu kuwa Mwokozi wetu. Hii ilikuwa sehemu muhimu sana ya mpango wa Mungu, na ni Yesu pekee ndiye angeweza kufanya hivyo.

Ufunuo 5

Shetani na kundi la watoto wa kiroho wakiondoka mbinguni.

Yohana pia aliona joka ambalo lilimwakilisha Shetani. Shetani hakupenda mpango wa Mungu. Alianzisha vita huko mbinguni. Wengi wa watoto wa kiroho wa Baba wa Mbinguni walikuwa na imani katika Yesu Kristo na walichagua kumfuata Yeye. Lakini baadhi yao walichagua kumfuata Shetani. Kwa sababu ya uchaguzi wao, iliwabidi waondoke mbinguni.

Ufunuo 12:3–11

Picha ya pamoja inayoonyesha askari wanaotembea, watu wenye shida, na njaa.

Yohana aliona kwamba Shetani na wafuasi wake waliendelea kupigana dhidi ya Yesu na wafuasi Wake duniani. Walijaribu kuwadanganya watu katika kutoamini injili ya Mwokozi. Kulikuwa na vita vingi, uharibifu, na magonjwa.

Ufunuo 6; 8–9; 12:17; 13:11–18; 17–18

Malaika Moroni akimwongoza Joseph Smith kwenye mabamba ya dhahabu.

Lakini Baba wa Mbinguni aliwatuma malaika kutoka mbinguni wakiwa na injili ya Yesu Kristo, ili iweze kuhubiriwa kwa kila mtu duniani.

Ufunuo 14:6–7

Familia ikishiriki sakramenti.

Baadhi ya watu wangeamini katika Yesu na kushika amri Zake, kama walivyofanya mbinguni. Ushuhuda wao juu ya Yesu ungewasaidia kushinda vita dhidi ya Shetani.

Ufunuo 12:11; 19:8–10

Yesu akishuka kutoka mbinguni, akiwa na malaika nyuma Yake.

Yohana aliona kwamba Yesu Kristo atakuja duniani tena. Atakuwa Mfalme wa ulimwengu wote. Shetani hatakuwa na nguvu tena. Kwa sababu ya Yesu, hakutakuwa na huzuni tena au maumivu. Watu wote wanaomwamini Yesu na kushika maagano pamoja Naye wataishi pamoja Naye na Baba wa Mbinguni milele.

Ufunuo 19:11–16; 20:1–2; 21:1–7