Yohana 1:43–51
Njoo Uone
Kumwalika rafiki kumfuata Yesu
Mtu aliyeitwa Filipo alikuwa mmoja wa wafuasi wa Yesu. Alijua kwamba Yesu alikuwa Mwokozi. Filipo alitaka Nathanaeli rafiki yake ajue pia kuhusu Yesu.
Yohana 1:43–45
Nathanaeli alijua kwamba maandiko yalisema Mungu angemtuma Mwokozi. Filipo alimwambia kwamba alikuwa amempata Mwokozi—jina Lake lilikuwa Yesu, kutoka Nazareti.
Yohana 1:45
Mwanzoni Nathanaeli hakumwamini. Hakufikiria kwamba Mwokozi angeweza kuwa wa kutoka Nazareti. “Laweza neno jema kutoka Nazareti?” aliuliza. Filipo alijibu, “Njoo uone.”
Yohana 1:46
Nathanaeli alienda na Filipo kukutana na Yesu. Wakati Yesu alipowaona wakija, Yeye alisema kwamba Nathanaeli alikuwa mtu mwema na mwaminifu. Nathanaeli alishangaa. Hakuwahi kukutana na Yesu hapo awali. Ni kwa jinsi gani Yesu alimjua?
Yohana 1:47–48
Yesu alimwambia Nathanaeli kwamba kabla ya Filipo kuzungumza naye, Yesu alikuwa amemwona amekaa chini ya mti wa mtini.
Yohana 1:48
Sasa Nathanaeli aliamini kwamba Yesu alikuwa Mwana wa Mungu. Yesu alimwambia Nathanaeli angeona mambo makubwa—kama malaika wakitoka mbinguni—yote kwa sababu ya imani yake.
Yohana 1:49–51