Mathayo 25:31–46
"Mmenitendea Mimi"
Tunapowatumikia wengine, tunamtumikia Yesu
Yesu Kristo aliwaambia wanafunzi Wake kwamba baada ya Yeye kurudi kwa Baba Yake wa Mbinguni, Yeye atarudi duniani pamoja na malaika wote watakatifu. Siku hiyo, watu kutoka mataifa yote watakusanyika mbele Yake—watu ambao walimfuata Yeye na watu ambao hawakumfuata.
Mathayo 25:31–33
Yesu atawaambia watu waliomfuata wangeweza kuingia katika ufalme Wake, kwa sababu alipokuwa na njaa, walimlisha. Yeye alipokuwa na kiu, walimpa Yeye kinywaji.
Mathayo 25:34–35
Walimpa Yeye nguo na mahali pa kukaa wakati Yeye alipohitaji. Yeye alipokuwa mgonjwa au gerezani, walimtembelea.
Mathayo 25:36
Watu watamwuliza Yesu wakati ni gani walifanya chochote kati ya vitu hivi vya ukarimu kwa ajili Yake. Mwokozi ataelezea kwamba tunapofanya mambo ya ukarimu kwa watu wengine, ni kama tunafanya mambo mazuri kwa niaba Yake.
Mathayo 25:37–40
Yesu atasema kwa watu ambao hawakumfuata Yeye kwamba hawawezi kuingia ufalme Wake. Yeye alipokuwa na njaa na kiu, hawakumpa Yeye chakula au kinywaji.
Mathayo 25:41–42
Hawakumsaidia wakati Yeye alipohitaji nguo au mahali pa kukaa. Yeye alipokuwa mgonjwa au gerezani, hawakumtembelea.
Mathayo 25:43
Yesu ataelezea kwamba tunapochagua kutomsaidia mtu mwenye shida, tunachagua kutomsaidia Yeye. Tunapochagua kuwasaidia wengine, tunachagua kumsaidia Yesu.
Mathayo 25:45