Matendo ya Mitume 12:1–17
Malaika Anamwachilia Huru Petro kutoka Gerezani
Mungu anajibu sala
Mfalme aliyeitwa Herodi hakuwapenda Wakristo. Alimuua Mtume Yakobo. Kisha akamweka Petro gerezani. Aliwaweka askari 16 kulinda gereza.
Matendo ya Mitume 12:1–4
Waumini wa Kanisa waliposikia haya, walisali na kusali kwa Baba wa Mbinguni kwa ajili ya Petro.
Matendo ya Mitume 12:5
Usiku mmoja, Petro alikuwa amelala. Alikuwa amefungwa na minyororo miwili katikati ya askari wawili.
Matendo ya Mitume 12:6
Ghafla, nuru ikang’ara gerezani, na malaika akatokea. “Inuka upesi,” malaika alisema, na minyororo ikaanguka kutoka mikononi mwa Petro. Malaika alimwambia Petro amfuate.
Matendo ya Mitume 12:7–8
Petro alidhani alikuwa anaota ndoto. Alimfuata malaika akiwapita walinzi. Lango la chuma ambalo liliongoza kwenda mjini lilifunguka lenyewe, na Petro na malaika wakapita.
Matendo ya Mitume 12:9–10
Malaika aliondoka, na Petro aligundua hakuwa anaota ndoto. Alijua Bwana alikuwa amemtuma malaika kumwokoa.
Matendo ya Mitume 12:10–11
Petro alikwenda nyumbani kwa mwanamke aliyeitwa Mariamu, mahali ambapo waumini wengi wa Kanisa walikuwa wamekutana humo kusali. Alibisha hodi mlangoni.
Matendo ya Mitume 12:12–13
Msichana aliyeitwa Roda alikuja mlangoni. Aliposikia sauti ya Petro, alifurahi sana! Alikimbia kwenda kuwaambia wengine.
Matendo ya Mitume 12:13–14
Wakati Roda alipomwambia kila mtu kwamba Petro alikuwa mlangoni, hawakumwamini. Petro aliendelea kubisha hodi.
Matendo ya Mitume 12:15–16
Hatimaye, walifungua mlango na kuona kwamba ilikuwa ni kweli. Petro alikuwa salama! Bwana alikuwa amejibu sala zao. Petro alimwambia kila mtu jinsi Bwana alivyomtoa gerezani.
Matendo ya Mitume 12:16–17