Hadithi za Maandiko
Yesu Anaingia Yerusalemu—Watu wanamkaribisha Mwokozi wao


Mathayo 21:1-16

Yesu Anaingia Yerusalemu

Watu wanamkaribisha Mwokozi wao

Watu wanasubiri kukutana na Yesu nje ya Yerusalemu.

Ilikuwa karibu wakati wa Pasaka, karamu muhimu kwa Wayahudi. Watu wengi walienda Yerusalemu kwa ajili ya Pasaka. Yesu na wanafunzi Wake walienda pia. Watu wengi waposikia kwamba Yesu alikuwa anakuja, walienda kumlaki.

Mathayo 21:1; Yohana 12:12–13

Yesu na wanafunzi Wake wakikaribia Yerusalemu.

Wakati Yesu na wanafunzi Wake walipokaribia Yerusalemu, Yeye aliwaomba wamlete punda Kwake. Miaka mingi kabla, nabii alikuwa amesema kwamba Mwokozi angekuja kwa unyenyekevu, akipanda punda mdogo.

Isaya 21:1–7; ona pia Zekaria 9:9.

Yesu anaingia Yerusalemu.

Yesu aliingia mjini akipanda punda. Mitume walikuwa na furaha sana kumwona Yeye. Walimkaribisha Yeye kama mfalme. Waliweka matawi ya mitende na nguo ardhini ili punda atembee juu yake. Walimshukuru Mungu na kusema kwa sauti, “Hosana: Mbarikiwa Mfalme wa Israeli ajaye katika jina la Bwana.”

Mathayo 21:8–9; Luka 19:36–38; Yohana 12:13

Watu wanamtazama Yesu.

Watu wengi katika Yerusalemu walijiuliza nini kilikuwa kinatendeka. “Ni nani huyu?” watu waliuliza. Wengine wakajibu kwamba alikuwa Yesu wa Nazareti.

Mathayo 21:10–11

Yesu anawaona watu wakibadilishana fedha hekaluni.

Kisha, Yesu alienda hekaluni Baadhi ya watu huko walikuwa wakibadilishana fedha na kuuza wanyama ili watolewe dhabihu. Yesu alijua walikuwa si waaminifu.

Mathayo 21:12

Yesu anawaambia watu wanaobadilishana fedha waondoke hekaluni.

Yesu hakupenda kwamba walikuwa wakijipatia pesa kutoka kwa watu waliotaka kuabudu hekaluni. Yeye aliwafanya waondoke hekaluni na kupindua meza zao. Yeye alisema, “Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; lakini mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.”

Mathayo 21:12–13; ona pia Isaya 56:7; Yeremia 7:11

Yesu anawaponya watu hekaluni.

Watu ambao walikuwa vipofu au ambao hawakuweza kutembea walimjia Yesu hekaluni, na Yeye aliwaponya. Watoto walisema kwa sauti “Hosana,” wakimsifu Yesu na kusema kwamba Yeye alikuwa Mwokozi.

Mathayo 21:14–15

Yesu anazungumza na makuhani na waandishi.

Baadhi ya makuhani na waandishi walikasirika walipoona kile Yesu alichofanya na kusikia kile watoto walichokuwa wakisema. Yesu aliwakumbusha kuhusu andiko ambalo linasema Mungu angefanya sifa kamilifu kuja kutoka vinywani mwa watoto.

Mathayo 21:15–16; ona pia Zaburi 8:2