Mathayo 25:1–13
Fumbo la Wanawali Kumi
Kuwa tayari kwa ajili ya Yesu kuja tena
Wanafunzi wa Yesu walijua kwamba siku moja, baada ya Yeye kurudi kwa Baba Yake, Yesu angerudi duniani. Walimwuliza jinsi ambavyo wangejua wakati Yeye atakaporudi. Walitaka kuwa tayari kwa ajili Yake. Ili kuwajibu, Yesu aliwambia fumbo.
Mathayo 24–3
Katika fumbo, wanawake kumi walikuwa wanakwenda kwenye harusi. Harusi ilikuwa usiku, hivyo wanawake walilazimika kuchukua taa zilizojaa mafuta ili ziangaze njia yao. Watano kati ya wanawake hao walikuwa na busara na walileta mafuta mengi. Wale watano wengine walikuwa wapumbavu na hawakuleta mafuta ya kutosha.
Mathayo 25:1–4
Wanawake walilazimika kumsubiria bwana harusi na kundi lake la harusi kuja. Lakini bwana harusi alichukua muda mrefu. Wakati wakisubiri, wote walilala.
Mathayo 24–5
Usiku wa manane, mtu alisema kwa sauti kwamba bwana harusi hatimaye alikuwa anakuja! Ilikuwa ni wakati wa wanawake kujiunga naye katika sherehe ya harusi.
Mathayo 25:6
Wanawake wote waliinua taa zao ili kuangaza njia yao. Lakini wanawake watano ambao hawakuleta mafuta ya kutosha hawakuwa na mwanga wowote. Mafuta yao yalikuwa yametumika wakati walipokuwa wakimsubiria bwana harusi.
Mathayo 25:7–8
Wanawake watano wasiokuwa na mafuta waliwaomba wengine kuwagawiya yao. Lakini hakukuwa na mafuta ya kutosha ya kugawana. Wanawake watano wasiokuwa na mafuta haraka walikwenda kununua zaidi.
Mathayo 25:8–9
Walipokuwa wameenda, bwana harusi akaja! Wanawake watano waliokuwa tayari walikwenda naye kwenye harusi hiyo.
Mathayo 25:10
Wakati wanawake wengine waliporudi, mlango ulikuwa umefungwa. Waligonga mlango na kuomba bwana harusi awaruhusu waingie ndani. Lakini walikuwa wamechelewa sana. Hawangeweza kuingia kwenye harusi.
Mathayo 25:11–12
Yesu ni kama bwana harusi katika fumbo. Hakuna ajuaye wakati Yeye atakapokuja tena. Ni Baba wa Mbinguni pekee anajua hilo. Kwa hivyo Yesu aliwaambia wafuasi Wake wawe tayari kama wanawake watano ambao walikuwa na mafuta ya kutosha. Watu wanaotii amri za Bwana na kumfuata Roho watakuwa tayari wakati Yesu Kristo atakapokuja tena.
Mathayo 24:36; 25:13; Mafundisho na Maagano 45:56–57