Timotheo 1 na 2
Barua kwa Timotheo
Paulo anamshauri rafiki yake kijana
Timotheo alikuwa kijana mwenye imani imara katika Yesu Kristo. Mama yake, Eunice, na bibi yake, Loisi, pia walikuwa wanawake wenye imani kubwa. Walimfundisha Timotheo kutoka kwenye maandiko, hata alipokuwa mtoto.
2 Timotheo 1:5; 3:15
Timotheo na Paulo walikuwa marafiki wazuri. Walikuwa wamefanya kazi na kusafiri pamoja, wakimtumikia Bwana na kuihubiri injili Yake. Paulo alimpenda Timotheo kama mwana.
Wafilipi 2:19–22; 1 Timotheo 1:2
Paulo alimwomba Timotheo kuliongoza Kanisa huko Efeso. Paulo alitakiwa kwenda mji mwingine. Wakati alipokuwa mbali, alimwandikia Timotheo barua ya kumsaidia.
1 Timotheo 1:1-3
Baadaye, wakati Paulo alipokuwa gerezani huko Rumi, alimwandikia Timotheo barua nyingine. Alimuonya Timotheo kwamba nyakati ngumu zingekuja. Baadhi ya watu wangegeuka kutoka kwenye ukweli na kupenda vitu vya ulimwengu zaidi kuliko Mungu. Wangefundisha vitu ambavyo si vya kweli.
2 Timotheo 3:1–7; 4:3–4
Paulo alimwambia Timotheo asiogope. Alisema, “Maana Mungu hakutupa Roho ya woga; bali ya nguvu, na ya upendo.” Paulo alimwambia Timotheo aendelee kufanya mambo aliyojifunza. Maandiko yangemwongoza kwa Yesu Kristo.
2 Timotheo 1:7–9; 3:14–17
Paulo alijua kwamba maisha yake punde yangefika mwisho. Lakini hakuogopa kufa. Paulo alimwambia Timotheo kwamba ingawa alikuwa amepitia changamoto nyingi katika maisha yake, alikuwa ameilinda imani yake imara. Aliamini kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wangempa uzima wa milele.
2 Timotheo 4:6–8