Hadithi za Maandiko
Barua kwa Timotheo—Paulo anamshauri rafiki yake kijana


Timotheo 1 na 2

Barua kwa Timotheo

Paulo anamshauri rafiki yake kijana

Timotheo akifundishwa na mama na bibi yake.

Timotheo alikuwa kijana mwenye imani imara katika Yesu Kristo. Mama yake, Eunice, na bibi yake, Loisi, pia walikuwa wanawake wenye imani kubwa. Walimfundisha Timotheo kutoka kwenye maandiko, hata alipokuwa mtoto.

2 Timotheo 1:5; 3:15

Paulo na Timotheo wakitembea pamoja. Paulo akiwa ameshikilia nguo ili kuwakinga na mvua.

Timotheo na Paulo walikuwa marafiki wazuri. Walikuwa wamefanya kazi na kusafiri pamoja, wakimtumikia Bwana na kuihubiri injili Yake. Paulo alimpenda Timotheo kama mwana.

Wafilipi 2:19–22; 1 Timotheo 1:2

Paulo akimwelekeza Timotheo kwenda Efeso ili kuliongoza Kanisa huko.

Paulo alimwomba Timotheo kuliongoza Kanisa huko Efeso. Paulo alitakiwa kwenda mji mwingine. Wakati alipokuwa mbali, alimwandikia Timotheo barua ya kumsaidia.

1 Timotheo 1:1-3

Timotheo akiwaangalia watu wakiikataa injili.

Baadaye, wakati Paulo alipokuwa gerezani huko Rumi, alimwandikia Timotheo barua nyingine. Alimuonya Timotheo kwamba nyakati ngumu zingekuja. Baadhi ya watu wangegeuka kutoka kwenye ukweli na kupenda vitu vya ulimwengu zaidi kuliko Mungu. Wangefundisha vitu ambavyo si vya kweli.

2 Timotheo 3:1–7; 4:3–4

Timotheo akifundisha kundi la Watakatifu kuhusu injili.

Paulo alimwambia Timotheo asiogope. Alisema, “Maana Mungu hakutupa Roho ya woga; bali ya nguvu, na ya upendo.” Paulo alimwambia Timotheo aendelee kufanya mambo aliyojifunza. Maandiko yangemwongoza kwa Yesu Kristo.

2 Timotheo 1:7–9; 3:14–17

Paulo akiwa gerezani huko Rumi.

Paulo alijua kwamba maisha yake punde yangefika mwisho. Lakini hakuogopa kufa. Paulo alimwambia Timotheo kwamba ingawa alikuwa amepitia changamoto nyingi katika maisha yake, alikuwa ameilinda imani yake imara. Aliamini kwamba Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wangempa uzima wa milele.

2 Timotheo 4:6–8