Hadithi za Maandiko
Kumtegemea Yesu Kristo kwa ajili ya Wokovu—Kuokolewa kwa neema Yake


Warumi 3:21–28; 5:1–11; 6:3–6

Kumtegemea Yesu Kristo kwa ajili ya Wokovu

Kuokolewa kwa neema Yake

Watu wakiwa wanabatizwa.

Watu kutoka sehemu nyingi tofauti walikuwa wakijiunga na Kanisa la Yesu Kristo. Waumini wa Kanisa waliitwa Watakatifu.

Warumi 1:7

Watu wawili wakizungumza kuhusu sheria ya Musa.

Baadhi ya Watakatifu walikuwa Wayahudi ambao bado walifuata sheria ya Musa. Wengine hawakuifuata. Hawakukubaliana kuhusu ikiwa walihitaji kuifuata sheria ya Musa.

Warumi 2:14–15, 23–29

Paulo akiandika barua.

Paulo alijua kwamba Watakatifu walikuwa na maswali haya. Aliandika barua kwa Watakatifu huko Rumi. Aliwaambia kwamba hakuna anayeweza kuokolewa kwa kujaribu tu kuifuata sheria ya Musa. Sisi sote tunatenda dhambi, alieleza. Ili kuokolewa, kila mtu anahitaji kuwa na imani katika Yesu Kristo na kumfuata Yeye.

Warumi 3:20–23

Watu wawili wakisoma barua ya Paulo.

Paulo alifundisha kwamba Mungu alimtuma Yesu Kristo ili ajichukulie juu Yake dhambi zetu. Kwa sababu ya dhabihu ya Yesu, sote tunaweza kutubu na kusamehewa dhambi zetu.

Warumi 3:24–31

Wanaume wawili wakishiriki sakramenti pamoja.

Paulo alifundisha kwamba Yesu Kristo anatupatia zawadi ya msamaha na nguvu ya kufanya mambo mema. Zawadi hii ya upendo inaitwa neema ya Yesu Kristo, na inatujaza kwa tumaini na shangwe. Paulo alisema kwamba tunapobatizwa, kama Yesu alivyobatizwa, ni kama kuanza maisha mapya kama mfuasi wa Yesu.

Warumi 5:1–11; 6:3–6