Hadithi za Maandiko
Silaha Zote za Mungu—Kubaki salama kiroho


Waefeso 6:11–17

Silaha Zote za Mungu

Kubaki salama kiroho

Paulo akiandika barua kwa Watakatifu katika Efeso kuhusu vita vyetu vya kiroho dhidi ya uovu.

Paulo aliwafundisha Watakatifu katika Efeso kwamba sote tuko katika vita vya kiroho dhidi ya uovu. Kama vile askari wanaovaa silaha ili kuiweka miili yao salama, tunaweza kuvaa silaha za kiroho za Mungu ili kuziweka salama roho zetu.

Waefeso 6:11–13

Msichana akiwa amevaa mkanda wa silaha.

Paulo alilinganisha silaha za askari na vitu ambavyo vinatulinda kiroho. Kwa mfano, alisema kwamba ukweli ni kama mkanda kuzunguka viuno vyetu.

Waefeso 6:14

Mvulana akivaa dirii ya kifua.

Kisha, Paulo alisema kwamba haki ni kama dirii ya kifua ambayo inalinda mioyo yetu.

Waefeso 6:14

Viatu na soksi za ulinzi.

Injili ya Yesu Kristo ya amani ni kama vile viatu tunavyovaa ili kuilinda miguu yetu.

Waefeso 6:15

Msichana akiwa amebeba ngao

Imani yetu katika Yesu Kristo ni kama ngao inayotulinda dhidi ya Shetani, kama vile ngao inavyowalinda askari kutokana na mishale ya adui zao.

Waefeso 6:16

Mvulana akiwa amevaa helmeti ya vazi la vita.

Paulo alisema kwamba wokovu ni kama helmeti ambayo inaweka vichwa vyetu na akili zetu salama.

Waefeso 6:17

Mapanga mawili.

Mwishowe, Paulo alisema kwamba Roho na neno la Mungu ni kama upanga.

Waefeso 6:17

Msichana na mvulana wakiwa wamelindwa kikamilifu kwa silaha za Mungu.

Tunapovaa kila kipande cha silaha za Mungu, tunaweza kusimama kwa ujasiri dhidi ya uongo na vishawishi vya ibilisi. Mungu alitupatia silaha hizi ili zitusaidie kuziweka roho zetu salama na imara.

Waefeso 6:11–13