Waefeso 6:11–17
Silaha Zote za Mungu
Kubaki salama kiroho
Paulo aliwafundisha Watakatifu katika Efeso kwamba sote tuko katika vita vya kiroho dhidi ya uovu. Kama vile askari wanaovaa silaha ili kuiweka miili yao salama, tunaweza kuvaa silaha za kiroho za Mungu ili kuziweka salama roho zetu.
Waefeso 6:11–13
Paulo alilinganisha silaha za askari na vitu ambavyo vinatulinda kiroho. Kwa mfano, alisema kwamba ukweli ni kama mkanda kuzunguka viuno vyetu.
Waefeso 6:14
Kisha, Paulo alisema kwamba haki ni kama dirii ya kifua ambayo inalinda mioyo yetu.
Waefeso 6:14
Injili ya Yesu Kristo ya amani ni kama vile viatu tunavyovaa ili kuilinda miguu yetu.
Waefeso 6:15
Imani yetu katika Yesu Kristo ni kama ngao inayotulinda dhidi ya Shetani, kama vile ngao inavyowalinda askari kutokana na mishale ya adui zao.
Waefeso 6:16
Paulo alisema kwamba wokovu ni kama helmeti ambayo inaweka vichwa vyetu na akili zetu salama.
Waefeso 6:17
Mwishowe, Paulo alisema kwamba Roho na neno la Mungu ni kama upanga.
Waefeso 6:17
Tunapovaa kila kipande cha silaha za Mungu, tunaweza kusimama kwa ujasiri dhidi ya uongo na vishawishi vya ibilisi. Mungu alitupatia silaha hizi ili zitusaidie kuziweka roho zetu salama na imara.
Waefeso 6:11–13