Hadithi za Maandiko
Yesu Anawabariki Watoto Wadogo—”Kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao”


Marko 10:13–16

Yesu Anawabariki Watoto wadogo

“Kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao”

Watu wanamwomba Yesu awabariki watoto wao.

Wakati Yesu alipokuwa akifundisha, baadhi ya watu waliwaleta watoto wao wadogo Kwake. Walimtaka Yesu awabariki watoto wao. Wanafunzi Wake walijaribu kuwakataza.

Mathayo 19:13; Marko 10:13

Yesu anawafundisha wanafunzi Wake kuwa kama watoto wadogo.

Yesu aliwaambia wanafunzi wawaache watoto waje Kwake. Yeye alisema kwamba watoto wadogo ni wa ufalme wa Mungu. Yeye alielezea kwamba kama mtu anataka kuishi na Mungu tena, anahitaji kuwa kama mtoto mdogo.

Mathayo 19:14; Marko 10:14–15

Yesu anawabariki watoto.

Kisha Yesu aliwachukua watoto wadogo mikononi Mwake na kuwabariki.

Mathayo 19:15; Marko 10:16