Hadithi za Maandiko
Kuishi kwa Imani katika Yesu Kristo—Yeye ni “mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu”


Waebrania 11–12

Kuishi kwa Imani katika Yesu Kristo.

Yeye ni “mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu.”

Mwanamume na msichana wakiangalia watu wakiharibu ufinyanzi wao.

Haikuwa rahisi daima kuwa mfuasi wa Yesu Kristo katika siku za mwanzo za Kanisa. Watu wakati mwingine waliwachukia waumini wa Kanisa au kuwafanyia mzaha kwa sababu ya imani yao. Paulo alitaka kuwasaidia kushika imani yao katika Yesu Kristo.

Waebrania 10:32–39

Mwanamume na msichana wakisali, Paulo akiwa upande wa mbele.

Paulo aliandika barua kwa Waebrania, au Wayahudi, Watakatifu. Alifundisha kwamba imani inamaanisha kuamini na kutumainia kitu fulani, hata kama hatuwezi kukiona. Kwa mfano, kuwa na imani katika Yesu Kristo inamaanisha kumwamini Yeye na ahadi Zake, hata kama bado hatujapokea baraka tunazozitumainia.

Waebrania 11:1, 6

Msichana akitabasamu wakati mwanamume akisoma hadithi kuhusu watu waliokuwa na imani.

Ili kuwasaidia Watakatifu wa Kiebrania kukabiliana na changamoto zao kwa imani, Paulo aliwakumbusha hadithi kuhusu watu katika maandiko ambao walikuwa na imani kubwa.

Waebrania 11:4–40

Nuhu akiangalia maelekezo ya kujenga safina.

Kwa mfano, Paulo alisimulia kumhusu Nuhu. Mungu alimwambia Nuhu ajenge safina ili kuiokoa familia yake kutokana na gharika. Nuhu alikuwa na imani ya kutii, hata kabla hajaiona mvua.

Waebrania 11:7

Ibrahimu na Sara wakiiacha nyumba yao.

Paulo aliwaambia kuhusu Ibrahimu na Sara, ambao walikuwa na imani ya kuondoka nyumbani kwao kwa sababu Mungu aliahidi kuwaongoza mahali pazuri zaidi. Pia walikuwa na imani katika ahadi ya Mungu kwamba wangekuwa na familia kubwa sana, ingawa walikuwa wazee na hawakuwa na watoto bado.

Waebrania 11:8–16

Mama na dada yake Musa wakimficha ndani ya kikapu.

Paulo pia alisimulia kuhusu mama yake Musa, Yokebedi. Alikuwa na imani ya kumficha Musa, wakati alipokuwa mtoto mchanga, ili kumweka salama dhidi ya mfalme mwovu.

Waebrania 11:23

Musa akimtazama Mmisri akimtendea vibaya Muisraeli.

Musa alikulia Misri. Angeweza kuwa tajiri na mwenye faraja. Lakini aliacha hayo yote kwa sababu alikuwa na imani katika Mungu na baraka Zake.

Waebrania 11:24–27

Musa akiigawanya Bahari ya Shamu.

Kwa sababu ya imani yake, Musa aliwaongoza watu wa Mungu kutoka utumwani. Walitembea hata kuvuka Bahari ya Shamu hadi kwenye nchi kavu!

Waebrania 11:29

Rahabu pamoja na watoto wake.

Paulo pia alisimulia kuhusu Rahabu. Alikuwa na imani ya kuwasaidia watu wa Mungu, ingawa hakuna yeyote katika mji wake aliyeamini katika Bwana. Imani yake iliiokoa familia yake.

Waebrania 11:30–31

Mwanamume na msichana wakitazama chungu walichokitengeneza.

Paulo alisema kwamba mifano hii mingi ya imani inaweza kutusaidia kuwa na imani katika Yesu Kristo pia, hata wakati ambapo maisha ni magumu. Tunaweza kutubu dhambi zetu na kumtegemea Yesu, “mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu.” Alikuwa tayari kufa kwa ajili yetu kwa sababu alijua kwamba Upatanisho Wake ungeleta shangwe kuu na uponyaji!

Waebrania 12:1–2