Hadithi za Maandiko
Yesu Anamponya Kipofu—Uponyaji ambao hutokea baada ya muda


Marko 8:22–25

Yesu Anamponya Kipofu

Uponyaji ambao hutokea baada ya muda

Watu wanamleta kipofu ili akaponywe na Yesu.

Katika mji ulioitwa Bethsaida, watu walimleta kipofu kwa Yesu. Walitaka Yesu ambariki ili aweze kuona.

Marko 8:22

Yesu akimbariki mtu yule.

Yesu aliushika mkono wa mtu huyo na kumwongoza kutoka nje ya mjini. Kisha Yesu akamwekea mtu huyo mikono yake na kumbariki.

Marko 8:23

Mtu huyo sasa anaweza kuona, lakini sio vizuri sana.

Yesu alimuuliza mtu yule kama ameeweza kuona kitu cho chote. Mtu huyo alitazama juu. Alisema aliweza kuona kidogo, lakini sio wazi kabisa. Alisema kwamba watu walionekana kama miti inayotembea.

Marko 8:23–24

Mtu huyo sasa anaweza kuona wazi.

Yesu alimbariki mtu yule tena. Wakati huu, alipotazama juu, kila kitu kilikuwa wazi. Yesu alikuwa amemponya!

Marko 8:25