Hadithi za Maandiko
Tabitha, Mwanamke “Aliyejaa Matendo Mema”—Alifufuliwa kwa uwezo wa Yesu Kristo


Matendo ya Mitume 9:36–42

Tabitha, Mwanamke “Aliyejaa Matendo Mema”

Alifufuliwa kwa uwezo wa Yesu Kristo

Tabitha akifuma nguo.

Tabitha alikuwa mwanafunzi mwaminifu wa Yesu Kristo. Aliishi katika mji kando ya bahari, uitwao Yafa. Alipenda kuwahudumia na kuwasaidia watu waliokuwa masikini.

Matendo ya Mitume 9:36

Tabitha akitoa nguo kwa watu walio katika shida.

Tabitha alitengeneza nguo na kuwapa wanawake walio katika shida. Walimpenda Tabitha.

Matendo ya Mitume 9:39

Tabitha anaugua.

Siku moja, Tabitha alikuwa mgonjwa sana. Alikuwa mgonjwa sana kiasi kwamba alikufa.

Matendo ya Mitume 9:37

Watu wawili wakiharakisha kuzungumza na Petro.

Waumini wengine wa Kanisa huko Yafa walihuzunika sana. Walijua kwamba Petro, mmoja wa Mitume wa Yesu, alikuwa katika mji uliokuwa karibu. Waliwatuma watu wawili kumwomba Petro aje kwao haraka.

Matendo ya Mitume 9:38

Watu wanamwongoza Petro kwenda kwa Tabitha.

Petro alikuja pale mwili wa Tabitha ulipokuwepo. Baadhi ya wanawake waliosaidiwa na Tabitha walikuwepo pale. Walimwonyesha Petro nguo alizozitengeneza kwa ajili yao.

Matendo ya Mitume 9:39

Petro anapiga magoti na kusali kando ya Tabitha.

Petro aliwaomba watu wote kuondoka chumbani. Alipiga magoti na kusali.

Matendo ya Mitume 9:40

Tabitha anafufuliwa.

Baada ya kusali, Petro alisema, “Tabitha, inuka.” Alifungua macho yake na akaketi kitako. Petro alimsaidia Tabitha kusimama. Alikuwa hai tena! Petro aliwaita marafiki zake waje na kumwona. Walistaajabu! Walijua alikuwa amefufuliwa kwa nguvu ya Yesu Kristo. Watu wengi zaidi walimwamini Yesu.

Matendo ya Mitume 9:40–42