Matendo ya Mitume 16:9–40
Paulo na Sila
Waliokolewa kwa miujiza kutoka kwa Bwana
Bwana aliwaita Paulo na Sila kuihubiri injili pamoja. Walisafiri kwenda miji mingi ili kuona jinsi makanisa yalivyokuwa yakiendelea.
Matendo ya Mitume 15:40–41; 16:4–8
Usiku mmoja, katika ono, Paulo alimwona mtu kutoka Makedonia akimwomba aje kwenye mji wake. Paulo na Sila waliondoka mara moja. Walijua Mungu aliwataka waende.
Matendo ya Mitume 16:9–10
Walipofika Makedonia, mwanamke aliyeitwa Lidia aliwasikia wakifundisha. Bwana alifungua moyo wa Lidia. Aliamini kile Paulo alichofundisha na akabatizwa.
Matendo ya Mitume 16:13–15
Lidia aliwaambia Paulo na Sila kwamba wangeweza kukaa nyumbani mwake wakati wakiwa huko.
Matendo ya Mitume 16:15
Lakini si kila mtu alipenda kwamba Paulo na Sila walikuwa pale. Baadhi ya watu hawakupenda kile walichokuwa wakikifundisha. Waliwapeleka Paulo na Sila sokoni na kuwaambia viongozi wa mji kwamba walikuwa wakisababisha matatizo.
Matendo ya Mitume 16:16–21
Watu waliwakasirikia Paulo na Sila. Viongozi wa mji walichana nguo za Paulo na Sila na kusema kwamba walipaswa kupigwa.
Matendo ya Mitume 16:22–23
Kisha viongozi wa mji waliwatupa Paulo na Sila gerezani. Waliwafunga miguu yao na kuwawekea ulinzi.
Matendo ya Mitume 16:23–24
Usiku ule, Paulo na Sila walisali na kuimba nyimbo kwa Mungu wakati wafungwa wengine wakiwasikiliza. Ghafla, ardhi ilianza kutikisika. Milango ya gereza ilifunguliwa, na kamba zilifunguliwa.
Matendo ya Mitume 16:25–26
Mlinzi aliamka na kuona milango iko wazi. Alifikiri wafungwa walikuwa wamekimbia na kwamba angekuwa katika matatizo kwa kuwaacha wakimbie. Paulo alimwambia mlinzi asiwe na shaka. Wafungwa wote walikuwa bado wako pale.
Matendo ya Mitume 16:27–28
Mlinzi alikuwa na hofu. Alipiga magoti kando ya Paulo na Sila na kusema, “Ninapaswa nifanye nini ili niokolewe?” Walisema, “Mwamini Bwana Yesu Kristo.”
Matendo ya Mitume 16:27–31
Paulo na Sila walimfundisha mlinzi na familia yake injili. Mlinzi alitibu majeraha ya Paulo na Sila. Usiku ule, yeye na familia yake walibatizwa.
Matendo ya Mitume 16:32–33