Hadithi za Maandiko
Watoto wa Nuru—Tukimwamini Yesu Kristo wakati tukimsubiri Yeye aje tena


Wathesalonike 1 na 2

Watoto wa Nuru

Kuamini katika Yesu Kristo wakati tukimsubiri Yeye aje tena

Paulo akiandika barua kwa watu huko Thesalonike.

Watakatifu katika wakati wa Paulo walifurahi kwa ajili ya siku ambayo Yesu Kristo angekuja tena duniani. Katika sehemu iliyoitwa Thesalonike, maisha yalikuwa yakizidi kuwa magumu kwa Watakatifu. Walijiuliza kama hii ilimaanisha Yesu angekuja karibuni. Paulo aliandika barua ili kuwasaidia.

1 Wathesalonike 4:16–18; 5:1–2; 2 Wathesalonike 1:4

Familia wakiwa wamelala.

Paulo alisema kwamba hakuna mtu anayejua ni lini Yesu atakuja tena. Itakuwa jambo la kushangaza kwa baadhi ya watu, kama mwizi anayekuja usiku wakati wamelala.

1 Wathesalonike 5:2–3; 2 Wathesalonike 2:2

Familia yenye furaha wakiwa wamekaa pamoja katika nuru angavu ya taa ya mafuta.

Lakini Paulo aliwaambia Watakatifu kwamba hawakuwa gizani. Kwa sababu walimfuata Yesu Kristo, Watakatifu walikuwa watoto wa nuru!

1 Wathesalonike 5:4–5

Familia yenye furaha wakishiriki injili na familia nyingine.

Paulo alieleza kwamba kabla ya Yesu kuja tena, watu wengi wangegeuka mbali na ukweli. Aliwataka Watakatifu, watoto wa nuru, waendelee kumfuata Yesu na kuendelea kutazamia ujio Wake. Tukifanya hivi, bila kujali kinachotokea ulimwenguni, tutakuwa tayari wakati Yesu atakaporudi.

1 Wathesalonike 1:5; 2 Wathesalonike 2:3