Wathesalonike 1 na 2
Watoto wa Nuru
Kuamini katika Yesu Kristo wakati tukimsubiri Yeye aje tena
Watakatifu katika wakati wa Paulo walifurahi kwa ajili ya siku ambayo Yesu Kristo angekuja tena duniani. Katika sehemu iliyoitwa Thesalonike, maisha yalikuwa yakizidi kuwa magumu kwa Watakatifu. Walijiuliza kama hii ilimaanisha Yesu angekuja karibuni. Paulo aliandika barua ili kuwasaidia.
1 Wathesalonike 4:16–18; 5:1–2; 2 Wathesalonike 1:4
Paulo alisema kwamba hakuna mtu anayejua ni lini Yesu atakuja tena. Itakuwa jambo la kushangaza kwa baadhi ya watu, kama mwizi anayekuja usiku wakati wamelala.
1 Wathesalonike 5:2–3; 2 Wathesalonike 2:2
Lakini Paulo aliwaambia Watakatifu kwamba hawakuwa gizani. Kwa sababu walimfuata Yesu Kristo, Watakatifu walikuwa watoto wa nuru!
1 Wathesalonike 5:4–5
Paulo alieleza kwamba kabla ya Yesu kuja tena, watu wengi wangegeuka mbali na ukweli. Aliwataka Watakatifu, watoto wa nuru, waendelee kumfuata Yesu na kuendelea kutazamia ujio Wake. Tukifanya hivi, bila kujali kinachotokea ulimwenguni, tutakuwa tayari wakati Yesu atakaporudi.
1 Wathesalonike 1:5; 2 Wathesalonike 2:3