Mathayo 4:1–10
Shetani Anamjaribu Yesu
Mfano wa kushinda majaribu
Baada ya ubatizo Wake, Yesu alienda nyikani ili kuwa na Mungu. Hakula kwa siku 40. Alikuwa akifunga na kusali ili kujiandaa kwa ajili ya misheni Yake.
Mathayo 4:1–2; ona Tafsiri ya Joseph Smith katika muhtasari 1b na 2c
Yesu alikuwa na njaa. Shetani alikuja na kumjaribu Yeye. Alisema kwamba kama Yesu alikuwa Mwana wa Mungu, angeweza kugeuza mawe kuwa mkate. Yesu asingefanya hivyo. Yesu alinukuu maandiko yanayosema kwamba Yeye aliishi kwa neno la Mungu, siyo mkate pekee.
Mathayo 4:2–4
Kisha Roho Mtakatifu alimpeleka Yesu juu ya kinara cha hekalu. Shetani alimjaribu Yesu aruke. Alisema kwamba ikiwa Yesu alikuwa Mwana wa Mungu, malaika wasingemwacha Yeye aumie. Yesu hakuruka. Yeye alimwambia Shetani kwamba maandiko yanasema hatupaswi kumjaribu Mungu.
Mathayo 4:5–7; ona Tafsiri ya Joseph Smith katika muhtasari 5a na 6a
Kisha, Roho Mtakatifu alimpeleka Yesu kwenye kilele cha mlima. Kutoka hapo, Yesu angeweza kuona falme zote za ulimwengu. Shetani alikuja na kusema kwamba angempa Yesu falme hizi zote kama angemsujudia.
Mathayo 4:8–10; ona Tafsiri ya Joseph Smith 8a
Yesu alimwambia Shetani kwamba maandiko yanasema tunapaswa kumsujudia Mungu pekee. Yesu alimwambia Shetani aondoke. Yesu alikwenda Galilaya kufundisha injili Yake. Yeye alijazwa na nguvu ya Roho Mtakatifu.
Luka 4:13–14