Luka 17:11–19
Yesu Anawaponya Wanaume Kumi Waliokuwa na Ukoma
Umuhimu wa shukrani
Yesu alipokuwa akisafiri, aliingia kijijini na kuwaona wanaume kumi ambao walikuwa na ugonjwa mbaya sana wa ngozi uitwao ukoma. Watu wenye ukoma walilazimika kukaa mbali na kila mtu, hata familia zao, hivyo hawakuwafanya watu wengine wawe wagonjwa.
Luka 17:11–12
Wanaume hawa walimwita Yesu na kumwomba awaponye. Yesu aliwaambia waende kwa makuhani katika mji. Ni makuhani tu ndio wangeweza kuamua kama wangeweza kuwa na watu wengine tena.
Luka 17:13–14; ona pia Mambo ya Walawi 14:2–3
Wanaume kumi wagonjwa walipokuwa wakitembea ili kuonana na makuhani, muujiza ulitokea. Ugonjwa wao ukatoweka. Walikuwa wameponywa!
Luka 17:14
Wakati mmoja wa wanaume alipoona kwamba ameponywa, aligeuka na kumshukuru Mungu kwa sauti kubwa. Alikuwa Msamaria.
Luka 17:15–16
Mtu yule alianguka miguuni pa Yesu kumshukuru kwa kile alichokifanya. Yesu aliuliza wako wapi wale watu wengine tisa walioponywa. Ni mtu mmoja tu aliyekuwa amerudi kumshukuru Yeye! Yesu kisha akamwambia, “Inuka enenda zako, imani yako imekuponya.”
Luka 17:16–19