Hadithi za Maandiko
Paulo Analinganisha Miili Yetu na Hekalu—Zawadi takatifu kutoka kwa Mungu


1 Wakorintho 6:16–20

Paulo Analinganisha Miili Yetu na Hekalu

Zawadi takatifu kutoka kwa Mungu

Paulo akiwafundisha watu huko Korintho kuhusu Yesu.

Korintho ulikuwa mji mkubwa kando ya bahari. Mji ulikuwa na watu wengi ambao hawakumwabudu Mungu. Paulo aliwafundisha watu katika Korintho kuhusu Yesu. Watu wengi waliamini na wakabatizwa.

Matendo ya Mitume 18:8–11

Baadhi ya watu hawafuati amri.

Baada ya Paulo kuondoka, alisikia kwamba waumini wa Kanisa walikuwa na matatizo fulani. Watu wengi katika Korintho hawakuwa wakifuata amri za Mungu kuhusu jinsi ya kuitendea au kuitumia miili yetu.

1 Wakorintho 6:13–18

Paulo akiandika barua kuelezea kwamba miili yetu ni kama mahekalu.

Paulo aliwaandikia barua. Alisema kwamba miili yetu ni kama hekalu la Mungu. Tunalitendea hekalu kwa heshima kwa sababu ni nyumba ya Mungu. Tunapaswa pia kuitendea miili yetu kwa heshima kwa sababu ni zawadi kutoka kwa Mungu.

1 Wakorintho 6:19–20

Familia ikiwa pamoja.

Baba wa Mbinguni anatutaka tuchague kufanya mambo mazuri kwa miili yetu. Tunapofanya hivyo, Roho Mtakatifu anaweza kuwa pamoja nasi.

1 Wakorintho 6:19

Familia ikizungumza kuhusu Upatanisho wa Yesu Kristo. Paulo akiwa mbele.

Paulo alisema kwamba Yesu Kristo alilipia gharama kwa ajili yetu kupitia kuteseka Kwake. Tunaonyesha upendo wetu kwa Yesu kwa kufanya chaguzi nzuri kuhusu miili yetu na kwa kushika amri Zake. Tunamwonyesha Mungu kwamba tunashukuru kwa zawadi nzuri ya miili yetu kwa kuitendea kama hekalu.

1 Wakorintho 6:20