Mathayo 12:1–12; Luka 13:10–17
Yesu Anamponya Mwanamke siku ya Sabato
Kutenda mema katika siku Yake takatifu
Yesu na wanafunzi Wake walikuwa wakitembea kupitia shamba la ngano siku ya Sabato. Walikuwa na njaa, kwa hivyo walivunja ngano na kuila. Baadhi ya viongozi wa Kiyahudi walioitwa Mafarisayo waliwaona. Mafarisayo walikuwa wametengeneza sheria nyingi kuhusu siku ya Sabato. Kuvunja ngano ilikuwa kinyume na sheria zao.
Mathayo 12:1–2
Mafarisayo walimwuliza Yesu kwa nini wanafunzi Wake hawakuiheshimu Sabato. Yesu alijibu kwamba hawakufanya kosa lolote. Mungu alitupa siku ya Sabato ili kutubariki, sio kufanya maisha yetu kuwa magumu zaidi.
Mathayo 12:2–8; Marko 2:27
Baadaye, Yesu alikuwa akifundisha katika sinagogi siku ya Sabato. Yesu alimwona mwanamke pale. Hakuweza kusimama wima. Alikuwa na tatizo hili kwa miaka 18.
Luka 13:10–12
Yesu Kristo alimwomba mwanamke aje Kwake. Yeye aliweka mikono Yake juu yake ili kumbariki.
Luka 13:12–13
Mara moja, yule mwanamke alisimama wima. Kiongozi wa sinagogi alighadhabika sana kwa sababu Yesu alikuwa akiponya siku ya Sabato.
Luka 13:13–14
Yesu alisema kwamba kumsaidia mwanamke huyu ilikuwa ni jambo sahihi kufanya. Ni sahihi kufanya mema siku ya Sabato. Kiongozi aliaibika, na watu katika sinagogi walifurahi kwa sababu yule mwanamke aliponywa.
Luka 13:15–17; ona pia Luka 6:9