Marko 12:41–44
Mjane na Sarafu Mbili Ndogo
Yesu Anafundisha kuhusu dhabihu
Yesu alienda hekaluni huko Yerusalemu. Yeye alipokuwa huko, Yeye alitazama watu wakitoa pesa kwa ajili ya kazi ya hekalu. Watu wengi matajiri walitoa pesa nyingi.
Marko 12:41
Kisha mjane maskini alitoa sarafu mbili zilizoitwa senti. Haikuwa nyingi sana, lakini ilikuwa pesa yote ambayo alikuwa nayo.
Marko 12:42, 44
Yesu alimwona mjane yule na kuwaomba wanafunzi Wake waje kuona kile alichokifanya.
Marko 12:43
Yesu alisema kwamba mjane huyo alikuwa ametoa zaidi ya mtu ye yote. Watu matajiri walikuwa wametoa pesa nyingi, lakini ilikuwa sehemu ndogo tu ya kile walichokuwa nacho. Mjane alitoa pesa kidogo tu, lakini alitoa yote aliyokuwa nayo.
Marko 12:43–44