Hadithi za Maandiko
Yesu Anabatizwa—Kuweka mfano wa utiifu kwa Mungu


Mathayo 3

Yesu Anabatizwa

Kuweka mfano wa utiifu kwa Mungu

Kielelezo cha Yohana Mbatizaji.

Mungu alimwita Yohana ili kuwasaidia watu kujiandaa kwa ajili ya ujio wa Yesu Kristo. Yohana aliwafundisha watu kutubu na kubatizwa. Watu walimwita yeye Yohana Mbatizaji.

Mathayo 3:1–12

Yesu akija kwa Yohana ili abatizwe.

Yohana alikuwa mwalimu mwenye ushawishi. Watu wengi walikuja kumsikiliza na kubatizwa. Siku moja, Yesu alikuja kubatizwa.

Mathayo 3:5, 13

Yesu na Yohana wakizungumza pamoja.

Yohana alijua kwamba Yesu daima alimtii Mungu. Hakuhitaji kutubu. Yohana hakufikiria kwamba alipaswa kumbatiza Yesu. Yohana alidhani Yesu alipaswa kumbatiza yeye!

Mathayo 3:14

Yohana akimbatiza Yesu

Yesu alisema kwamba Yeye pia alihitaji kubatizwa. Yeye alitaka kutii amri zote za Baba Yake. Yeye pia alitaka kuweka mfano kwa ajili yetu. Yohana alimbatiza.

Mathayo 3:13–15; 2 Nefi 31:5–7

Yesu anabatizwa. Roho Mtakatifu alishuka.

Baada ya Yesu kutoka majini, Roho Mtakatifu alimshukia kama njiwa. Baba wa Mbinguni alizungumza kutoka mbinguni, akisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa.” Baba wa Mbinguni alikuwa na furaha sana juu ya Yesu.

Mathayo 3:16–17