Mathayo 3
Yesu Anabatizwa
Kuweka mfano wa utiifu kwa Mungu
Mungu alimwita Yohana ili kuwasaidia watu kujiandaa kwa ajili ya ujio wa Yesu Kristo. Yohana aliwafundisha watu kutubu na kubatizwa. Watu walimwita yeye Yohana Mbatizaji.
Mathayo 3:1–12
Yohana alikuwa mwalimu mwenye ushawishi. Watu wengi walikuja kumsikiliza na kubatizwa. Siku moja, Yesu alikuja kubatizwa.
Mathayo 3:5, 13
Yohana alijua kwamba Yesu daima alimtii Mungu. Hakuhitaji kutubu. Yohana hakufikiria kwamba alipaswa kumbatiza Yesu. Yohana alidhani Yesu alipaswa kumbatiza yeye!
Mathayo 3:14
Yesu alisema kwamba Yeye pia alihitaji kubatizwa. Yeye alitaka kutii amri zote za Baba Yake. Yeye pia alitaka kuweka mfano kwa ajili yetu. Yohana alimbatiza.
Mathayo 3:13–15; 2 Nefi 31:5–7
Baada ya Yesu kutoka majini, Roho Mtakatifu alimshukia kama njiwa. Baba wa Mbinguni alizungumza kutoka mbinguni, akisema, “Huyu ni Mwanangu mpendwa.” Baba wa Mbinguni alikuwa na furaha sana juu ya Yesu.
Mathayo 3:16–17