Hadithi za Maandiko
Amefufuka—Yesu Kristo anashinda mauti kwa ajili ya wote


Luka 24:1–12, 36–49; Yohana 20

Amefufuka

Yesu Kristo anashinda mauti kwa ajili ya wote

Wanafunzi wa Yesu wanaondoka kaburini Kwake.

Wanafunzi wa Yesu waliuweka mwili Wake kaburini. Walitaka kufanya zaidi kuutunza mwili Wake, lakini ilikuwa karibu Sabato. Walipanga kurudi baada ya Sabato kumaliza.

Luka 23:52–56

Mariamu Magdalena na wengine wanarudi kaburini.

Mapema asubuhi siku ya tatu baada ya kifo cha Yesu, Mariamu Magdalena na wengine walikwenda kaburini.

Luka 24:1; Yohana 20:1

Mwili wa Yesu haupo kaburini.

Walipofika, waliona kwamba jiwe lililofunika kaburi lilikuwa limevingirishwa mbali. Walikwenda kaburini, na mwili wa Yesu haukuwepo.

Luka 24:2–3; Yohana 20:1

Mariamu anawaambia Petro na Yohana kwamba mtu ameuchukua mwili wa Yesu.

Mariamu alikimbia kuwaambia Petro na Yohana kwamba mtu alikuwa ameuchukua mwili wa Yesu. Petro na Yohana walikimbilia kaburini.

Yohana 20:2–4

Petro na Yohana wanaona kwamba mwili wa Yesu haupo kaburini.

Walipofika kaburini, Petro na Yohana waliingia ndani. Waliona kwamba mwili wa Yesu ulikuwa haupo. Kitambaa ambacho Yeye alikuwa amefunikwa nacho bado kilikuwa pale.

Yohana 20:5–7

Mariamu anawaona malaika wawili kaburini.

Petro na Yohana walienda nyumbani, lakini Mariamu alikaa kaburini, akilia. Alitazama kaburini na kuona malaika wawili. Walimwuliza kwa nini alikuwa akilia. Alisema mtu alikuwa ameuchukua mwili wa Yesu, na hakujua pale ulipo.

Yohana 20:11–13

Yesu anamwuliza Mariamu kwa nini analia.

Kisha Yesu akaja, lakini Mariamu hakujua ilikuwa ni Yeye. Yesu alimwuliza, "Mama, unalilia nini?" Mariamu alifikiri Yeye alikuwa mtunza bustani. Alimuuliza kama alijua pale mwili wa Yesu ulipokuwa.

Yohana 20:14–15

Mariamu anageuka na kumwona Yesu.

Yesu alisema, "Mariamu." Mariamu aligeuka. Sasa alijua kwamba alikuwa ni Yesu! Mariamu alisema Kwake, "Bwana." Yesu alimwomba awaambie wanafunzi wengine kwamba Yeye alihitaji kwenda kwa Baba Yake wa Mbinguni. Mariamu aliwapata wanafunzi wengine na kuwaambia kwamba alikuwa amemwona Yesu na Yeye alikuwa hai tena!

Yohana 20:16–18

Yesu anatokea na anaongea na Mitume Wake.

Jioni ile, wengi wa Mitume walikuwa pamoja. Walifunga milango, wakiogopa kwamba viongozi wa Wayahudi wangejaribu kuwatafuta. Ghafla, walimwona Yesu akiwa amesimama miongoni mwao. Mwanzoni waliogopa. Walidhani Yeye alikuwa ni roho. Yesu alisema, "Amani iwe kwenu."

Luka 24:33–38; Yohana 20:19

Mmoja wa Mitume anagusa mkono wa Yesu.

Yesu aliwaalika Mitume kugusa mikono na miguu Yake. Yeye aliwataka wajue kwamba Yeye alikuwa na mwili, sio tu roho. Hata alikula samaki na asali pamoja nao. Wanafunzi walikuwa na furaha sana kumwona Yeye!

Luka 24:39–44; Yohana 20:20

Yesu anafundisha kuhusu kifo Chake na Ufufuo Wake.

Kisha Yesu aliwasaidia Mitume Wake kuelewa maandiko ambayo yalifundisha kuhusu kifo Chake na Ufufuko Wake. Yeye aliwataka wamfundishe kila mtu kwamba kwa sababu Yake, wangeweza kutubu na kusamehewa. Mitume wangekuwa mashahidi Wake.

Luka 24:44–48

Tomaso anazungumza na Mitume wengine wawili.

Mtume Tomaso hakuwepo wakati Yesu alipokuja. Alisema asingeamini kwamba Yesu alikuwa hai isipokuwa aweze kuona alama za misumari mikononi Mwake.

Yohana 20:24–25

Yesu anatokea tena.

Siku nane baadaye, wanafunzi walikusanyika pamoja. Yesu alitokea tena. Wakati huu Tomaso alikuwa pale.

Yohana 20:26

Tomaso anapiga magoti mbele ya Yesu.

Yesu alimwalika Tomaso kugusa majeraha katika mikono yake na ubavuni Mwake. Yeye alimwambia Tomaso, "Wala usiwe asiyeamini, bali aaminiye." Tomaso alisema, "Bwana wangu na Mungu wangu." Sasa Tomaso aliamini kwamba Yesu alifufuka. Yesu alisema kwamba watu wanabarikiwa wanapoamini, hata kama hawajamwona Yeye.

Yohana 20:27–29