Mathayo 26:36–46; Luka 22:39–46
Yesu akiwa Gethsemane
Akiteseka kwa ajili ya dhambi za ulimwengu
Yesu na Mitume Wake walienda kwenye bustani ya Gethsemane. Yesu aliwaomba Petro, Yakobo, na Yohana wamfuate na kuwaambia wengine wasubiri.
Mathayo 26:36-37; Yohana 18:1
Yesu aliwaambia Petro, Yakobo, na Yohana kwamba Alikuwa anajisikia huzuni sana. Aliwaomba wabaki macho pamoja Naye wakati Akisali.
Mathayo 26:38
Kisha Yesu akaenda mbali kidogo ndani ya bustani. Alianza kuteseka kwa ajili ya dhambi zetu ili kwamba sisi tuweze kutubu na kusamehewa. Yesu pia alijisikia maumivu yetu yote, magonjwa, na huzuni ili aweze kujua jinsi ya kutusaidia. Alifanya hivi kwa sababu Yeye anatupenda. Hii yote ilikuwa sehemu ya mpango wa Baba wa Mbinguni.
Mathayo 26:39; Luka 22:41; Warumi 3:23; Alma 7:11–13; 3 Nefi 27:19
Mateso ya Yesu yalikuwa na maumivu makali kiasi kwamba alimwomba Baba wa Mbinguni kama angeweza kumwondolea mateso hayo. Lakini alikuwa tayari kufanya kile Baba Yake alichomtaka Yeye afanye. Alisema, “Walakini si Mapenzi Yangu, bali Yako Yatendeke”
Luka 10:42
Yesu alienda kwa Petro, Yakobo, na Yohana na kuona kwamba walikuwa wamelala. Aliwaamsha na kuwaomba tena wabaki macho na kusali. Lakini alijua kwamba japokuwa walitaka kubaki macho, walikuwa wamechoka sana.
Mathayo 26:40–41
Yesu alisali tena. Malaika alikuja Kumpa nguvu. Alisikia uchungu mwingi, na alisali hata kwa bidii zaidi. Jasho lake lilikuwa matone ya damu yaliyoanguka ardhini.
Mathayo 26:42; Luka 22:43–44; Mosia 3:7; Mafundisho na Maagano 19:16–19
Mara mbili zaidi, Yesu alikwenda kwa Petro, Yakobo, na Yohana na kuwakuta wamelala. Mwishowe, Aliwaamsha, kwa sababu muda ulikuwa umefika wa Yeye kuchukuliwa.
Mathayo 26:43–46