Hadithi za Maandiko
Yesu Anafundisha kuhusu Udongo, Mbegu, Mkate, na Lulu—Hadithi rahisi za kutusaidia kuelewa kweli za kiroho


Mathayo 13

Yesu Anafundisha kuhusu Udongo, Mbegu, Mkate, na Lulu

Hadithi rahisi za kutusaidia kuelewa kweli za kiroho

Yesu akifundisha kutoka kwenye mashua wakati watu wakisikiliza.

Yesu mara nyingi alisimuliwa hadithi zinazoitwa mafumbo. Katika mafumbo, Yesu alifananisha mambo ya kawaida, ya kila siku na kweli muhimu kuhusu injili Yake. Ili kuelewa mafumbo, wafuasi Wake walilazimika kusikiliza kwa makini na kufikiria kwa kina kuhusu maana yake. Mafumbo yaliwasaidia kujifunza kuhusu ufalme wa Mungu.

Mathayo 13: 3, 10–15

Yesu anaanza fumbo kuhusu mtu aliyepanda baadhi ya mbegu.

Katika fumbo moja, mtu alikwenda shambani kupanda mbegu kadhaa. Alitawanya mbegu nyingi kote shambani. Mbegu zilianguka kwenye aina tofauti za ardhi.

Mathayo 13:3

Baadhi ya mbegu zinaanguka kwenye njia ngumu ya mchanga.

Baadhi ya mbegu zilianguka kwenye njia ngumu ya mchanga, ambapo kamwe hazingeweza kuota. Ndege walikuja na kula mbegu ambazo zilianguka huko.

Mathayo 13:4

Baadhi ya mbegu zinaanguka katika udongo wenye miamba.

Baadhi ya mbegu zilianguka kwenye udongo wenye miamba. Mbegu zilimea kwa kasi, lakini mizizi haikuweza kukua kwa sababu ya miamba. Ilipokuwa joto, mimea ilikufa.

Mathayo 13:5–6

Baadhi ya mbegu zinaanguka kwenye udongo ambao umejaa magugu.

Baadhi ya mbegu zilianguka kwenye udongo uliojaa magugu ya miiba. Kwa sababu ya magugu ya miiba, mbegu hazikuweza kuota.

Mathayo 13:7

Baadhi ya mbegu zinakua na kuwa mimea imara.

Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri. Zikawa mimea imara, yenye afya. Zilizaa matunda mengi.

Mathayo 13:8

Yesu anaelezea kwamba mbegu ni kama neno la Mungu.

Ili kuwasaidia wanafunzi Wake kuelewa, Yesu alielezea kile fumbo Lake lilichomaanisha. Mbegu ni kama neno la Mungu. Aina tofauti za udongo ni kama mioyo ya watu na namna tofauti tofauti wanavyoitikia kwenye kusikia neno la Mungu. Udongo mzuri ni kama watu wanaosikia neno la Mungu, kulielewa, na kumtii Yeye.

Mathayo 13:18–23

Yesu anafundisha kuhusu mbegu ya haradali.

Ili kufundisha kuhusu jinsi ambavyo ufalme wa Mungu ungekua, Yesu alisimulia kuhusu mbegu ya haradali. Ni ndogo sana, lakini hukua na kuwa mti ambapo ndege wanaweza kuishi.

Mathayo 13:31–32

Yesu anafundisha kuhusu mkate na chachu.

Yesu pia alisema kwamba ufalme wa Mungu ni kama hamira au chachu ambayo mwanamke aliitumia wakati akitengeneza mkate. Inachukua chachu kidogo tu kufanya kinyunya kizima kuvimba.

Mathayo 13:33

Yesu anaelezea fumbo kuhusu lulu.

Yesu alisimulia hadithi nyingine kuhusu mtu aliyenunua lulu. Alipata moja ambayo ilikuwa nzuri sana na yenye thamani. Aliuza kila kitu alichokuwa nacho ili aweze kununua lulu. Yesu alisimulia hadithi hii kufundisha kwamba baraka za injili ni za thamani sana kiasi kwamba tunapaswa kufanya kila kitu tunachoweza ili kuzipokea.

Mathayo 13:45–46