Mathayo 13
Yesu Anafundisha kuhusu Udongo, Mbegu, Mkate, na Lulu
Hadithi rahisi za kutusaidia kuelewa kweli za kiroho
Yesu mara nyingi alisimuliwa hadithi zinazoitwa mafumbo. Katika mafumbo, Yesu alifananisha mambo ya kawaida, ya kila siku na kweli muhimu kuhusu injili Yake. Ili kuelewa mafumbo, wafuasi Wake walilazimika kusikiliza kwa makini na kufikiria kwa kina kuhusu maana yake. Mafumbo yaliwasaidia kujifunza kuhusu ufalme wa Mungu.
Mathayo 13: 3, 10–15
Katika fumbo moja, mtu alikwenda shambani kupanda mbegu kadhaa. Alitawanya mbegu nyingi kote shambani. Mbegu zilianguka kwenye aina tofauti za ardhi.
Mathayo 13:3
Baadhi ya mbegu zilianguka kwenye njia ngumu ya mchanga, ambapo kamwe hazingeweza kuota. Ndege walikuja na kula mbegu ambazo zilianguka huko.
Mathayo 13:4
Baadhi ya mbegu zilianguka kwenye udongo wenye miamba. Mbegu zilimea kwa kasi, lakini mizizi haikuweza kukua kwa sababu ya miamba. Ilipokuwa joto, mimea ilikufa.
Mathayo 13:5–6
Baadhi ya mbegu zilianguka kwenye udongo uliojaa magugu ya miiba. Kwa sababu ya magugu ya miiba, mbegu hazikuweza kuota.
Mathayo 13:7
Mbegu zingine zilianguka kwenye udongo mzuri. Zikawa mimea imara, yenye afya. Zilizaa matunda mengi.
Mathayo 13:8
Ili kuwasaidia wanafunzi Wake kuelewa, Yesu alielezea kile fumbo Lake lilichomaanisha. Mbegu ni kama neno la Mungu. Aina tofauti za udongo ni kama mioyo ya watu na namna tofauti tofauti wanavyoitikia kwenye kusikia neno la Mungu. Udongo mzuri ni kama watu wanaosikia neno la Mungu, kulielewa, na kumtii Yeye.
Mathayo 13:18–23
Ili kufundisha kuhusu jinsi ambavyo ufalme wa Mungu ungekua, Yesu alisimulia kuhusu mbegu ya haradali. Ni ndogo sana, lakini hukua na kuwa mti ambapo ndege wanaweza kuishi.
Mathayo 13:31–32
Yesu pia alisema kwamba ufalme wa Mungu ni kama hamira au chachu ambayo mwanamke aliitumia wakati akitengeneza mkate. Inachukua chachu kidogo tu kufanya kinyunya kizima kuvimba.
Mathayo 13:33
Yesu alisimulia hadithi nyingine kuhusu mtu aliyenunua lulu. Alipata moja ambayo ilikuwa nzuri sana na yenye thamani. Aliuza kila kitu alichokuwa nacho ili aweze kununua lulu. Yesu alisimulia hadithi hii kufundisha kwamba baraka za injili ni za thamani sana kiasi kwamba tunapaswa kufanya kila kitu tunachoweza ili kuzipokea.
Mathayo 13:45–46