“Familia ya Yanagida,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)
“Familia ya Yanagida,” Hadithi za Mafundisho na Maagano
1950–1951
Familia ya Yanagida
Zaka na imani katika Yesu Kristo.
Toshiko na Tokichi Yanagida waliishi huko Japani. Waliamini katika Yesu Kristo na walikuwa wamejiunga na Kanisa Lake. Lakini maisha nchini Japani yalikuwa magumu wakati huo. Vita vilikuwa vimeharibu nyumba nyingi na majengo mengi. Toshiko na Tokichi walitaka kujenga nyumba kwa ajili ya familia yao, lakini walikuwa masikini sana.
Watakatifu, 3:543
Akina Yanagida walijua Bwana aliwataka kulipa zaka, lakini hawakuwa na uhakika kwamba wangeweza. Toshiko alimuuliza mmisionari wanapaswa kufanya nini. “Zaka ni ngumu sana kwetu,” alisema. Mmisionari aliahidi kwamba kama wangelipa zaka yao, Bwana angewasaidia kufikia lengo lao la kumiliki nyumba.
Mafundisho na Maagano 119; Watakatifu, 3:543–44
Toshiko na Tokichi hawakuwa na uhakika. Kwa shida walipata pesa za kutosha kununua chakula cha mchana kwa ajili ya mwana wao shuleni. Lakini waliamua kumwamini Bwana na kulipa zaka.
Saints, 3:543-44
Bwana aliibariki familia ya Yanagida. Punde waliweza kununua ardhi na kuanza kujenga nyumba.
Watakatifu, 3:544
Siku moja mkaguzi alikuja. Alisema kulikuwa na tatizo katika ardhi yao, na hawangeweza kujenga nyumba hapo. Aliwaambia wajenzi kusimamisha ujenzi.
Watakatifu, 3:544
Akina Yanagida walikuwa na huzuni sana. Waliwaambia wamisionari kilichotokea. Wamisionari walisema wangefunga na kusali pamoja na akina Yanagida.
Watakatifu, 3:545
Baadaye, mkaguzi mwingine alikuja. Alisema tatizo la ardhi yao linaweza kurekebishwa. Akina Yanagida wangeweza kujenga nyumba yao. “Ninyi wawili lazima mmefanya kitu kizuri,” yule mkaguzi aliwaambia Toshiko na Tokichi. Walijua Mungu alikuwa amewabariki. Walifurahi kwamba walikuwa wamemwamini Yeye na kulipa zaka.
Watakatifu, 3:545