Hadithi za Maandiko
Jela ya Liberty


“Jela ya Liberty,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)

“Jela ya Liberty,” Hadithi za Mafundisho na Maagano

Oktoba 1838–Machi 1839

Jela ya Liberty

Kumpata Bwana wakati wa nyakati ngumu

Askari wakiwafukuza Watakatifu huko Missouri nje ya nyumba zao.

Watu wengi walioishi Missouri hawakuwapenda Watakatifu. Gavana aliwatuma askari ili kuwafanya waondoke. Askari waliwafukuza Watakatifu kutoka majumbani mwao, waliiba vitu kutoka kwenye nyumba zao, na kuwajeruhi wengi wao.

Saints, 1:355–56, 362, 364

Askari wakiwakamata Joseph Smith na viongozi wengine wa Kanisa.

Askari waliwakamata Nabii Joseph Smith na viongozi wengine wa Kanisa.

Saints, 1:357–58

Mwana wa Joseph Smith akilia wakati Joseph akitwaliwa kama mfungwa.

Joseph aliuliza kama angeweza kuwa na muda peke yake na familia yake. Askari walisema hapana. Walimchukua Joseph na wafungwa wengine.

Saints, 1:366

Joseph akiwaambia walinzi kuacha kuzungumza.

Usiku mmoja, Joseph na wafungwa wengine walisikiliza wakati walinzi wao wakicheka kuhusu mambo mabaya waliyokuwa wamewafanyia Watakatifu. Joseph hangeweza kuvumilia kusikia tena. Alisimama na kupiga kelele, “Nyamazeni!” Aliongea kwa nguvu za Mungu. Walinzi waliogopa. Walisema walisikitika na kuacha kuzungumza.

Saints, 1:367–68

Joseph na marafiki zake katika Jela ya Liberty

Baadaye, Joseph na rafiki zake waliwekwa jela katika mji ulioitwa Liberty. Jela ilikuwa baridi sana, ndogo, na yenye giza. Walikuwa tu na majani machafu kulala. Kulikuwa na chakula kidogo tu, na kiliwafanya wagonjwa.

Saints, 1:369–70, 374, 384–85

Joseph akiwa na wasiwasi kuhusu Watakatifu.

Joseph alifikiria mengi kuhusu Watakatifu. Na aliwapenda wao. Alikuwa na wasiwasi juu yao. Lakini hakuweza kufanya chochote kuwasaidia.

Saints, 1:385–86

Joseph akisali katika Jela la Liberty

Joseph alisali sana. Alimuuliza Mungu alikuwa wapi na kwa nini hakuwasaidia Watakatifu. Je, Mungu alikuwa amesahau kumhusu yeye na Kanisa?

Mafundisho na Maagano 121:1–6

Joseph akipokea jibu la maombi yake.

Mungu alijibu sala ya Joseph. Yeye alisema, “Mwanangu, amani iwe katika nafsi yako.” Yeye alimwambia Joseph kwamba changamoto zake hazitadumu milele, na zingekuwa kwa faida yake. Mungu alimkumbusha Joseph kwamba Yesu Kristo alikuwa amepitia hata mambo magumu zaidi. Yeye aliahidi kwamba angekuwa pamoja na Joseph “milele na milele.”

Mafundisho na Maagano 121:7; 122:5–9