Hadithi za Maandiko
Parley Anaomba Msamaha


“Parley Anaomba Msamaha,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)

“Parley Anaomba Msamaha,” Hadithi za Mafundisho na Maagano

Januari–Julai 1837

Parley Anaomba Msamaha

Ushuhuda wa rafiki unajenga imani yake

Thankful na Parley Pratt wakimbeba mtoto wao mchanga.

Ilipofika wakati kwa Thankful na Parley Pratt kupata mtoto wao, walirudi nyumbani kutoka misheni yao huko Kanada. Walikuwa na mtoto wa kiume mwenye afya kama vile Bwana alivyowaahidi.

Saints, 1:270

Parley akiwa amembeba mtoto kaburini kwa Thankful.

Kwa huzuni, Thankful alifariki saa chache baada ya mtoto kuzaliwa. Parley alijua asingeweza kumtunza mtoto bila yeye. Alimwomba mwanamke huko Kirtland amtunze mtoto wakati akirudi Kanada kumaliza misheni yake.

Saints, 1:270

Joseph Smith akizungumza na watu kuhusu benki mpya.

Huko Kirtland, Joseph Smith alianzisha benki kupata fedha kwa ajili ya kazi ya Mungu. Aliwaomba watu kuiruhusu benki kutumia fedha zao ili wengine waweze kuikopa. Lakini, kwa sababu nyingi, benki haikuwa na pesa za kutosha na ilibidi ifungwe. Benki nyingine nchini Marekani zilikuwa zikianguka pia.

Saints, 1:260–61, 264–68

Watakatifu wakibishana kuhusu benki hiyo ndani ya Hekalu la Kirtland.

Maisha yakawa magumu kwa Watakatifu. Baadhi walipoteza kazi zao na sasa hawakuwa na pesa za kutosha kununua chakula au nguo. Baadhi ya watu walimkasirikia Joseph, hata baadhi ya marafiki zake wa karibu. Walidhani Joseph hakuwa nabii wa kweli kwa sababu benki ilianguka.

Saints, 1:264–68, 272275

Parley akiwa amemshikilia mtoto wake mchanga.

Wakati haya yakitokea, Parley alirudi nyumbani kutoka misheni yake. Matatizo ya benki yalifanya maisha kuwa magumu kwa Parley pia. Hangekuwa na pesa za kutosha kulipia nyumba yake, na asingekuwa na mahali pa kuishi.

Saints, 1:270–71

Parley akimwandikia barua Joseph.

Sasa Parley alimkasirikia Joseph pia. Alimwandikia Joseph barua. Alimwambia Joseph kwamba bado aliamini katika Kitabu cha Mormoni. Lakini pia alisema mambo yasiyo ya ukarimu kuhusu Nabii. Alimwambia Joseph kuwa kwanza alikuwa amekosea kuanzisha benki.

Saints, 1:271

Parley akiwasalimu marafiki kutoka Kanada.

Baadaye, baadhi ya marafiki wa Parley kutoka Kanada walikuja Kirtland. Parley alikuwa amewafundisha injili, na walikuwa na furaha ya kumwona tena.

Saints, 1:279–80

Marafiki wa Parley wakiangalia wakati Parley na wengine wakibishana na Joseph.

Lakini pia walishangazwa kwamba Parley na wengine wengi walikuwa wamepoteza imani yao kwamba Joseph Smith alikuwa nabii.

Saints, 1:279–80

Parley akizungumza na John Taylor.

Mmoja wa marafiki wa Parley kutoka Kanada alikuwa John Taylor. Wakati Parley alipomwona, alimwambia John jinsi alivyomkasirikia Joseph Smith. Alimwambia John asimfuate tena Joseph.

Saints, 1:280

John akishiriki ushuhuda wake na Parley.

John alimkumbusha Parley kwamba walipokuwa Kanada, Parley alikuwa ameshiriki ushuhuda wake kwamba Joseph Smith alikuwa nabii wa kweli. “Sasa nina ushuhuda ule ule,” John alisema. “Kama kazi ilikuwa kweli miezi sita iliyopita, ni kweli leo. Kama Joseph Smith alikuwa nabii hapo mwanzo, basi hata sasa yeye ni nabii.”

Saints, 1:280

Parley akimtazama Joseph na wengine ndani ya Hekalu la Kirtland.

Parley alijua rafiki yake John alikuwa sahihi. Alihuzunika kuhusu barua yake ya hasira kwa Joseph. Alijua kwamba Joseph alikuwa akifanya kwa uwezo wake wote kufanya kazi ya Bwana. Matatizo ya benki hayakumaanisha kwamba Joseph hakuwa nabii wa kweli wa Yesu Kristo.

Saints, 1:283

Parley akiomba radhi kwa Joseph.

Parley alikwenda nyumbani kwa Joseph. Alimwambia Joseph kwamba alihuzunika kuhusu mambo yasiyo ya ukarimu aliyosema. Joseph alimsamehe Parley, akasali kwa ajili yake, na akambariki. Parley alihudumu misheni nyingi zaidi na kuwaambia watu ulimwenguni kote kwamba Joseph Smith alikuwa nabii wa Bwana.

Mafundisho na Maagano 64:7–11; Saints, 1:283