Hadithi za Maandiko
Misheni ya Parley kwenda Kanada


“Misheni ya Parley kwenda Kanada,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)

“Misheni ya Parley kwenda Kanada,” Hadithi za Mafundisho na Maagano

Aprili–Juni 1836

Misheni ya Parley kwenda Kanada

Kuonyesha imani katika ahadi za Bwana

Viongozi wa Kanisa wakitembea karibu na Hekalu la Kirtland.

Mara baada ya Hekalu la Kirtland kuwekwa wakfu, viongozi wengi wa Kanisa walikwenda misheni kuhubiri injili.

Mafundisho na Maagano 88:81; 109:22–23; 112:28–29; Saints, 1:249

Parley Pratt akiwa amekaa kando ya kitanda cha mkewe.

Parley Pratt alipenda kushiriki injili. Lakini alidhani alipaswa kukaa nyumbani kwa sababu mke wake, aliyeitwa Thankful, alikuwa mgonjwa. Pia hawakuwa na pesa nyingi.

Saints, 1:249

Heber Kimball akimbariki Parley na Thankful.

Heber Kimball, rafiki wa Parley na mmoja wa Mitume, alikuja kumtembelea. Alimpa Parley baraka na kusema alipaswa kuhubiri injili huko Kanada. Katika baraka, Heber aliahidi kwamba Thankful angepata nafuu. Aliahidi angepata mwana na Bwana angemsaidia Parley kupata pesa alizohitaji.

Saints, 1:249–50

Parley akisema kwaheri kwa Thankful.

Thankful na Parley walikuwa wameoana kwa miaka 10. Hawakuwa na mtoto hata mmoja. Lakini walikuwa na imani katika ahadi za Bwana. Japokuwa ingekuwa vigumu kuwa mbali na Thankful huko Kanada, Parley aliondoka ili kushiriki injili.

Saints, 1:250

Parley akiwa kwenye misheni yake huko Kanada.

Huko Canada, Parley alitafuta sehemu ambazo angeweza kuwafundisha watu. Aliuliza kama angeweza kufundisha katika makanisa na majengo mengine. Kila mtu alisema hapana.

Saints, 1:252–53

Parley anakutana na John na Leonora Taylor.

Kisha Parley akakutana na John na Leonora Taylor. Walimpenda Yesu Kristo na Biblia. John alimuuliza Parley kama kile alichofundisha kilikuwa tofauti na Biblia.

Saints, 1:252–53

Parley na John wakizungumza.

Parley alisema alifundisha kuhusu Yesu, manabii, ubatizo, na Roho Mtakatifu. Mambo hayo yote yalikuwa katika Biblia. John aliuliza “Je, nini kuhusu Joseph Smith na Kitabu cha Mormoni?“ Parley alimwambia John kwamba yeye alijua Kitabu cha Mormoni kilikuwa cha kweli, kama vile Biblia, na kwamba Joseph Smith alikuwa nabii wa Mungu.

Saints, 1:253

Parley akifundisha kikundi cha Watakatifu.

John aliamini kile Parley alichosema. Alisoma Kitabu cha Mormoni na kuamini kilikuwa cha kweli. John na Leonora waliwaalika marafiki zao Joseph, Mercy, na Mary Fielding na wengine kuja kusikia Parley akifundisha. Watu wengi walibatizwa na kujiunga na Kanisa.

Saints, 1:254–55

Parley akisema kwaheri kwa marafiki zake huko Kanada.

Parley alikuwa na furaha, lakini alitaka kwenda nyumbani kwa Thankful huko Kirtland. Alisema kwaheri kwa marafiki zake wapya nchini Kanada. Alipokuwa akisalimiana nao kwa mikono kuwaaga, walimpatia fedha za kumsaidia kuitunza familia yake.

Saints, 1:255–56

Parley na Thankful wakiwa pamoja huko Kanada.

Wakati Parley alipofika nyumbani, aligundua kwamba Thankful alikuwa akijisikia vizuri zaidi. Parley alipata nakala zaidi za Kitabu cha Mormoni na kurudi Kanada ili kuendelea kushiriki injili. Wakati huu, Thankful alikwenda pamoja naye.

Saints, 1:256

Parley na Thankful wakikumbatiana

Punde Thankful na Parley aligundua kwamba wangepata mtoto. Walikumbuka baraka ambazo Heber alikuwa amempa Parley. Walihisi kama kila kitu Bwana alichokuwa ameahidi katika baraka hiyo kilikuwa kinakuja kuwa kweli.

Saints, 1:256