“Ndoa ya Mitala,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)
“Ndoa ya Mitala,” Hadithi za Mafundisho na Maagano
1831–1890
Ndoa ya Mitala
Amri kwa muda
Wakati Nabii Joseph alipokuwa akijifunza Biblia, alisoma kuhusu manabii kama Ibrahimu na Musa ambao walikuwa wameoa na zaidi ya mke mmoja. Joseph alikuwa na maswali mengi. Hivyo aliamua kusali na kumuuliza Bwana.
Mafundisho na Maagano 132:1; Saints, 1:121, 503
Bwana alisema kwamba kwa kawaida mwanaume alipaswa kuwa na mke mmoja tu. Lakini wakati mwingine Bwana alimwamuru mtu kuoa mke zaidi ya mmoja. Hii iliitwa ndoa ya mitala. Bwana alimwambia Joseph kwamba watu Wake wanapaswa kuwa tu katika ndoa za mitala kama Yeye ataamuru.
Yakobo 2:27–30; Mafundisho na Maagano 132:34–39; Saints, 1:121, 290–91, 489–90, 503
Miaka kadhaa baadaye, Bwana alimwambia Joseph na baadhi ya Watakatifu wengine kuwa katika ndoa za mitala. Haikuwa rahisi kuishi amri hii.
Saints, 1:290–91, 444–46
Serikali ilitoa sheria dhidi ya ndoa za mitala. Baadhi ya Watakatifu, ikijumuisha viongozi wa Kanisa, waliwekwa gerezani.
Saints, 2:501–4
Mnamo 1890, Bwana alimwambia Wilford Woodruff, Rais wa Kanisa, kwamba wanaume wasioe tena zaidi ya mke mmoja. Viongozi wa Kanisa walishiriki amri hii na Watakatifu. Hii bado ni amri ya Bwana leo—mwanaume lazima aoane na mke mmoja tu.
Tamko Rasmi 1; Saints, 2:598–601, 607–9