Hadithi za Maandiko
Telii Anamtumikia Bwana


“Telii Anamtumikia Bwana,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)

“Telii Anamtumikia Bwana,” Hadithi za Mafundisho na Maagano

Aprili 1844–Machi 1852

Telii Anamtumikia Bwana

Kujenga Kanisa huko Tubuai

Telii na wengine wakiwatazama wamisionari Watakatifu wa Siku za Mwisho wakiwasili.

Mwanamke aliyeitwa Telii aliishi katika kisiwa kidogo kilichoitwa Tubuai. Wamisionari kutoka makanisa tofauti wakati mwingine walimtembelea Tubuai, lakini kwa kawaida hawakukaa kwa muda mrefu. Siku moja mnamo 1844, Telii alifurahi kusikia kwamba wamisionari kutoka Kanisa la Yesu Kristo la Watakatifu wa Siku za Mwisho walikuwa wamewasili Tubuai.

Mafundisho na Maagano 1:1; 133:8

Telii na Nabota wanawaalika wamisionari kukaa nao.

Wamisionari walikuwa njiani kuelekea kwenye baadhi ya visiwa vikubwa. Lakini watu wa Tubuai waliwataka kukaa na kufundisha injili. Telii na mumewe, Nabota, walisema wamisionari wangeweza kukaa nyumbani mwao. Mmoja wa wamisionari, Addison Pratt, alikubali.

Saints, 1:573–74

Telii na Nabota wakishiriki chakula na mmoja wa wamisionari.

Telii na Nabota walishiriki kila kitu walichokuwa nacho na Addison. Walimfundisha kuzungumza lugha yao. Addison aliwafundisha kuhusu Yesu Kristo.

Telii akibatizwa wakati Nabota akiangalia.

Roho Mtakatifu aliwaambia Telii na Nabota kwamba injili ya Mwokozi ni ya kweli. Walikuwa watu wa kwanza kubatizwa Tubuai.

Saints, 1:573–74

Telii na wengine wakishiriki injili na watu katika Tubuai.

Telii, Nabota, na Addison wakawa marafiki wakubwa. Walisafiri pamoja na kufundisha injili huko Tubuai na visiwa vingine. Wakati watu walipojaribu kuwaambia Watakatifu huko Tubuai kwamba hawapaswi kujiunga na Kanisa, Telii aliwafundisha kutoka kwenye maandiko kwamba Kanisa ni la kweli.

Saints, 2:27, 45

Telii, Nabota, na Watakatifu wengine wanaimba pamoja.

Telii alitaka kuwasaidia watu wengi zaidi huko Tubuai kujifunza injili ya Yesu Kristo. Aliweka maandiko kwenye muziki na kualika makundi makubwa kuimba pamoja naye jioni. Kuimba nyimbo za Telii kuliwasaidia watu wengi kujifunza kutoka kwenye maandiko na kukumbuka kile walichojifunza.

Mafundisho na Maagano 25:12

Telii na familia yake wakiikaribisha familia ya Addison.

Miaka kadhaa baadaye, wamisionari zaidi walikuja Tubuai, ikijumuisha familia ya Addison. Telii aliwakaribisha nyumbani kwake. Alifanya kazi na mke wa Addison, Louisa, kuwahudumia wanawake wa Tubuai.

Saints, 2:133–34

Telii na familia yake wakiendelea kushiriki injili na wengine.

Baada ya muda, wamisionari walilazimishwa kuondoka Tubuai na visiwa vingine. Lakini Telii aliendelea kufundisha na kuwaongoza Watakatifu. Kwa sababu ya mfano na huduma ya Telii, Kanisa huko Tubuai lilibaki imara.

Saints, 2:150–51