“Lucy Morley na Familia Yake,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)
“Lucy Morley na Familia Yake,” Hadithi za Mafundisho na Maagano
Novemba 1830
Lucy Morley na Familia Yake
Wengi wanaamini na kubatizwa
Siku moja, Lucy Morley mwenye umri wa miaka 15 alikuwa akimsaidia jirani yake, Abigail Daniels, kufuma nguo. Walipokuwa wakifanya kazi, walisikia hodi mlangoni. Walikuwa ni wamisionari watatu. Abigail aliwakaribisha waingie ndani. Walisema kwamba Yesu Kristo alikuwa amewatuma kushiriki ujumbe.
Saints, 1:102–3
Wanaume wale waliwaambia Abigail na Lucy kwamba Yesu alikuwa amemwita Joseph Smith kuwa nabii. Pia waliwaambia kuhusu Kitabu cha Mormoni.
Saints, 1:103
Kwa mshangao wa Lucy, Abigail alikasirika. Aliwafukuza wamisionari kuondoka nyumbani kwake.
Saints, 1:103
Lucy alijua wamisionari hawa walikuwa watumishi wa Mungu. Aliwaambia waitembelee familia yake inayoishi mtaaa unaofuata. “Baba yangu anaishi maili moja kutoka hapa,” alisema. “Nendani huko na mtalishwa na kutunzwa.”
Saints, 1:103–4
Lucy alikuwa sahihi. Wamisionari walipata chakula kizuri katika shamba la familia ya Morley. Wazazi wa Lucy walikuwa marafiki wa Sidney Rigdon. Waliamini Yesu aliwataka kushiriki kila kitu walichokuwa nacho kwa wengine. Waliwaalika wamisionari kuwafundisha wao na marafiki zao.
Saints, 1:104
Usiku ule, majira ya usiku wa manane, watu 17 walibatizwa. Katika siku chache zilizofuata, watu 50 zaidi walikuja kwenye shamba la Morley kuwasikiliza wamisionari, na wakaomba kubatizwa. Hata rafiki yake Lucy Abigail Daniels alibadilisha mawazo yake kuhusu wamisionari. Yeye na mumewe waliamua kujiunga na Kanisa.
Saints, 1:105; Mafundisho na Maagano 20:25, 37