Hadithi za Maandiko
Misheni kwa Waamerika Wenyeji


“Misheni kwa Waamerika Wenyeji,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)

“Misheni kwa Waamerika Wenyeji,” Hadithi za Mafundisho na Maagano

Oktoba 1830–Januari 1831

Misheni kwa Waamerika Wenyeji

Wahindi wa Delaware wanasikia injili

Parley Pratt, Oliver Cowdery, na wamisionari wengine wakitembelea nyumba ya Wahindi wa Delaware.

Mara baada ya Parley Pratt kubatizwa, Bwana alimwita kuungana na Oliver Cowdery na wengine katika misioni. Aliwataka wahubiri injili kwa Waamerika Wenyeji. Wamisionari walisafiri kwa wiki nyingi kupitia theluji nyingi. Hatimaye, walikutana na Kikthawenund, chifu wa Wahindi wa Delaware.

Mafundisho na Maagano 28:14; 30:5–6; 32; Saints, 1:98, 115

Oliver na Parley wakishiriki ujumbe wa Kitabu cha Mormoni.

Chifu alikuwa rafiki kwa wamisionari. Aliwaalika marafiki zake kusikia ujumbe wao. Oliver alisema yeye na Parley walikuwa wamesafiri umbali mrefu ili kuwaletea Kitabu cha Mormoni. Kitabu hicho kinasimulia juu ya watu ambao waliishi katika mabara ya Amerika miaka mingi iliyopita. Mungu aliwataka kushiriki kitabu hicho ili kila mtu aweze kujua kuhusu Yesu Kristo.

Saints, 1:115-16

Oliver akitoa nakala ya Kitabu cha Mormoni kwa Kikthawenund.

Oliver alimpatia Kikthawenund nakala ya Kitabu cha Mormoni. Alikuwa mwenye shukrani kwamba Oliver na marafiki zake walikuwa wamekuja kutoka mbali sana kushiriki Kitabu cha Mormoni kwa watu wake. Aliwaambia Oliver na Parley kwamba aliwataka warudi kuwasomea na kuwafundisha zaidi kuhusu Kitabu cha Mormoni.

Saints, 1:116–17