“Ndoa ya Milele na Familia,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)
“Ndoa ya Milele na Familia,” Hadithi za Mafundisho na Maagano
1843–1846
Ndoa ya Milele na Familia
Kuunganishwa kwa nguvu ya Yesu Kristo
Wakati Emma na Joseph walipofunga ndoa, waliamini ndoa yao ingeisha watakapokufa. Hivi ndivyo ndoa zote zilivyokuwa. Lakini kisha Bwana alimwambia Joseph kwamba ndoa na familia zingeweza kudumu milele.
Watakatifu, 1:413
Bwana alimfundisha Joseph kuhusu ndoa ya milele. Kupitia nguvu ya ukuhani, mwanaume na mwanamke wanaweza kufanya agano na Bwana. Kama watashika agano lao, Bwana anaahidi kwamba ndoa yao itadumu milele. Hii inaitwa kuunganishwa. Punde, Joseph na Emma waliunganishwa milele.
Mafundisho na Maagano 132:7, 19–24; Watakatifu, 1:413, 432–33, 481–82, 492, 502–3
Joseph pia alijifunza kwamba wakati mwanaume na mwanamke wanapounganishwa, watoto wao wangeunganishwa kwao. Kwa sababu ya nguvu ya Yesu Kristo, familia yao ingeweza kudumu milele. Wakati Joseph alipowaambia Watakatifu kuhusu baraka hii, walikuwa na furaha sana! Hawangeweza kusubiri kuunganishwa pamoja.
Mafundisho na Maagano 131:2; 132:6–7; Watakatifu; 1: 492–93, 580
Bwana baadaye alifundisha kwamba kuunganishwa kunapaswa kufanywa ndani ya hekalu. Watakatifu walifanya kazi kwa bidii ili kumaliza hekalu huko Nauvoo ili waweze kuunganishwa pamoja. Wakati hekalu lilipokuwa tayari, familia nyingi ziliunganishwa. Waliunganishwa hata na wanafamilia ambao walikuwa wamefariki. Walikuwa na shukrani kwa ajili ya baraka hii!
Watakatifu, 1:579–80