Hadithi za Maandiko
Susa Young Gates na Joseph F. Smith


“Susa Young Gates na Joseph F. Smith,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)

“Susa Young Gates na Joseph F. Smith,” Hadithi za Mafundisho na Maagano

1902–1918

Susa Young Gates na Joseph F. Smith

Ufunuo kuhusu ulimwengu wa roho

Brigham Young akiongea na binti yake Susa.

Susa Young Gates alikuwa binti wa Brigham Young. Alizaliwa Utah na kukulia huko. Alipenda kuandika, na alipenda kuhudumu katika Kanisa la Bwana.

Saints, 3:9–10, 64

Susa akipokea baraka ya ukuhani

Wakati Susa alipokuwa mtu mzima, aliugua sana. Aliomba baraka ya ukuhani. Katika baraka, Bwana alimwambia Susa Yeye alimtaka afanye kazi ya hekalu.

Saints, 3:193–94

Susa akizungumza na mwanamke mwingine kuhusu mahekalu na historia ya familia.

Baada ya baraka, Susa alijisikia vizuri. Alitumia muda wake kujifunza kuhusu historia ya familia yake. Alipowapata wanafamilia waliofariki bila kubatizwa, alikwenda hekaluni kubatizwa kwa niaba yao. Alipenda kuwaambia watu kuhusu kazi ya historia ya familia. Kwa huzuni, watu wengi hawakupendezwa.

Saints, 3:194–95, 206

Susa akizungumza na Joseph F. Smith.

Siku moja, Susa alimtembelea rafiki yake Joseph F. Smith, Rais wa Kanisa. Rais Smith alikuwa mgonjwa kwa wiki nyingi. Susa alijua kwamba alikuwa na huzuni sana kwa sababu mwanawe alikuwa amefariki. Alikuwa na huzuni kuhusu mambo mengine yanayotokea ulimwenguni pia, kama vita na magonjwa.

Saints, 3:197–99, 205–6

Joseph F. Smith anamwambia Susa kuhusu ono lake.

Lakini Susa alipoketi chini na Rais Smith, alifurahi kuzungumza naye. Alimwambia Susa kwamba Mungu amempa ono maalum. Ilikuwa yote kuhusu ulimwengu wa roho, ambapo watu huenda baada ya kufariki. Ono lake liliandikwa kwenye karatasi. Rais Smith alimpa Susa na kumuomba asome.

Saints, 3:206–7

Susa akisoma kuhusu ono.

Susa alisoma karatasi ile. Ilisema kwamba Yesu Kristo alitembelea ulimwengu wa roho. Alimtuma Adamu, Hawa, na wanaume na wanawake wengine waaminifu kufundisha roho ambao hawakupokea injili walipokuwa hai. Walikuwa wakisaidia roho hizi kujiandaa ili watu waweze kubatizwa kwa niaba yao hekaluni.

Mafundisho na Maagano 138:11–19, 29–48; Saints, 3:206–7

Joseph F. Smith na Susa wakizungumza.

Susa alishangazwa aliposoma ono la Rais Smith. Rais Smith alitabasamu kwake. “Susa,” alisema, “utafanya kazi kubwa.” Alimwambia kwamba alimpenda kwa ajili ya imani yake katika Bwana.

Saints, 3:206

Susa ameketi karibu na Hekalu la Salt Lake.

Susa aliandika kuhusu ufunuo katika shajara yake. “Ee, ilikuwa faraja kwangu!” alisema. Hakuweza kungoja kuwaambia rafiki zake na waumini wengine wa Kanisa kuhusu hilo. Alijua ono la Rais Smith lingewasaidia Watakatifu kufurahia kufanya kazi ya hekaluni kwa watu katika ulimwengu wa roho.

Saints, 3:207