“Samuel Smith Anashiriki Kitabu cha Mormoni,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)
“Samuel Smith Anashiriki Kitabu cha Mormoni,” Hadithi za Mafundisho na Maagano
1830–1832
Samuel Smith Anashiriki Kitabu cha Mormoni
Kitabu kimoja kinabariki maisha ya wengi
Bwana alimwita Samuel Smith, kaka mdogo wa Joseph, katika misheni ya kushiriki injili. Samweli alikutana na John na Rhoda Greene na kuwaambia kuhusu Kitabu cha Mormoni. John alikuwa mhubiri katika kanisa lingine. Alisema kwamba atachukua nakala ya kitabu na kuona kama mtu yeyote katika kanisa lake alitaka kukisoma.
Saints, 1:99
Baada ya miezi michache, Samweli alirudi. Rhoda alisema mumewe hakuweza kumpata mtu yeyote aliyetaka kusoma Kitabu cha Mormoni. Alimrudishia Samweli.
Saints, 1:99
Samuel alihuzunika. Aligeuka kuondoka, lakini Rhoda alimsimamisha. Alisema kwamba alikuwa amesoma Kitabu cha Mormoni, na alikipenda.
Saints, 1:99
Roho Mtakatifu alimwambia Samweli arudishe kitabu hicho kwa Rhoda. “Muombe Mungu akupe ushuhuda,” Samweli alimwambia. Alimfundisha Rhoda kuhusu Roho Mtakatifu na jinsi ambavyo angejua kwamba Kitabu cha Mormoni ni cha kweli.
Moroni 10:3–5; Saints, 1:99–100
Samweli alirudi nyumbani kutoka kwenye misheni yake. Hakuwa amembatiza mtu yeyote, na watu wachache tu walipendezwa na Kitabu cha Mormoni.
Rhoda na John waliomba, na Roho Mtakatifu aliwaambia Kitabu cha Mormoni ni cha kweli. Kisha Rhoda alishiriki kitabu hicho na kaka yake, Brigham Young.
Saints, 1:100
Brigham na rafiki yake, Heber Kimball, walikuwa wakitafuta Kanisa la kweli la Yesu. Walikisoma Kitabu cha Mormoni. Walijifunza na kusali kuhusu injili ya Yesu Kristo kwa takribani miaka miwili.
Wakati huu, Brigham na Heber walikwenda kwenye mikutano ya Kanisa pamoja na familia zao. Katika mojawapo ya mikutano hii, Brigham alimsikia mmisionari akishiriki ushuhuda wake. Mmisionari hakuwa mnenaji mzuri, lakini Brigham alihisi Roho Mtakatifu wakati mmisionari alipokuwa akizungumza. Brigham alijua alikuwa anasema ukweli.
Brigham, Heber, na wake zao, Miriam na Vilate, walibatizwa. Walimpenda Mwokozi na injili Yake. Miaka kadhaa baadaye, Bwana alimwita Brigham na Heber kuwa Mitume Wake na kuhudumu misheni. Kwa sababu Samweli alishiriki Kitabu cha Mormoni, watu wengi walijiunga na Kanisa la Mwokozi.
Mafundisho na Maagano 124:127–29; 126; Saints, 1:215–16