“Kukusanyika Ohio,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)
“Kukusanyika Ohio,” Hadithi za Mafundisho na Maagano
Desemba 1830–Mei 1831
Kukusanyika Ohio
Imani ya Lucy Smith na muujiza
Huko Ohio, watu wengi zaidi na zaidi walikuwa wakijiunga na Kanisa. Bwana aliwaambia Joseph Smith kwamba Watakatifu wanaoishi katika maeneo mengine wanapaswa kukusanyika Ohio. Ingeweza kuwa safari ndefu. Lakini Bwana aliahidi kwamba baada ya kukusanyika, Yeye angewafundisha Watakatifu sheria Yake na kuwabariki kwa uwezo wa kufanya kazi Yake.
Mafundisho na Maagano 37; 38:32; Saints, 1:109–110
Mama yake Joseph, Lucy, na kundi la takriban waumini wa Kanisa 80 waliacha nyumba zao huko New York na kuhamia Ohio. Walipanda kwenye mashua ambayo ingewabeba sehemu ya safari. Baada ya kusafiri kwa siku chache, mashua ilibidi isimame. Barafu nene ndani ya maji ilizuia njia yao.
Saints, 1:121–22
Watakatifu iliwabidi wasubiri barafu ivunjike vipande. Walikuwa wamechoka, walikuwa na njaa, walilowana na wenye kuona baridi.
Saints, 1:122
Ilikuwa ni vigumu kusubiria. Baadhi ya Watakatifu walianza kubishana wao kwa wao.
Saints, 1:122
Lucy hakupenda kuwasikia Watakatifu wakibishana. Alijua alihitaji kusema kitu. “Imani yenu iko wapi?” aliuliza. Lucy aliwaambia Watakatifu kwamba kama wangeomba kwa Mungu, Yeye angevunja barafu ili waweze kuendelea na safari yao.
Saints, 1:122–23
Ghafla, walisikia kelele kama radi wakati barafu ilipovunjika. Njia ilifunguliwa ndani ya ile barafu, pana ya kutosha kwa ajili ya mashua yao kupita.
Saints, 1:123
Watakatifu walishangazwa na kuwa na shukrani. Walikusanyika kusali na kumshukuru Baba wa Mbinguni. Mashua yao ilisafiri salama kuelekea Ohio.
Saints, 1:123
Wakati Watakatifu walipofika Ohio, waumini wa Kanisa huko waliwakaribisha na kuwasaidia kupata sehemu za kuishi. Bwana alitimiza ahadi Yake kuwafundisha sheria Yake na kuwapa uwezo wa kufanya kazi Yake.
Mafundisho na Maagano 42; Saints, 1:126