Hadithi za Maandiko
Ufunuo kwa ajili ya Emma


“Ufunuo kwa ajili ya Emma,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)

“Ufunuo kwa ajili ya Emma,” Hadithi za Mafundisho na Maagano

Julai 1830

Ufunuo kwa ajili ya Emma

Aliteuliwa na Bwana ili kufanya kazi Yake

Joseph akipunga mkono wa kwaheri kwa Emma

Maisha yalikuwa yakibadilika haraka sana kwa Emma na Joseph. Bwana alimwambia Joseph kwamba anapaswa kuacha kufokasi kwenye kilimo. Badala yake, Joseph anapaswa kutumia muda wake kuwafundisha watu kuhusu Yesu Kristo na kusaidia Kanisa la Bwana kukua.

Mafundisho na Maagano 24:7–9; Saints, 1:96

Emma akitazama nje dirishani wakati Joseph akiondoka.

Emma alikuwa na maswali mengi kuhusu badiliko hili. Hakujua kile alichopaswa kufanya wakati Joseph alipokuwa akimtumikia Bwana. Je, yeye pia angemsaidia Bwana na Kanisa Lake?

Saints, 1:96

Emma na Joseph wakitabasamu

Bwana aliongea na Emma kupitia ufunuo uliotolewa kwa Joseph. Alimwita “Emma Smith, binti yangu.” Alimwambia Emma kwamba alikuwa amemteua na kumwita kufanya kazi Yake. Alikuwa mwanamke maalumu, na alikuwa na mambo makubwa ya yeye kufanya.

Mafundisho na Maagano 25:1–3

Emma akishiriki injili

Bwana alimwomba Emma kusafiri pamoja na Joseph. Bwana alisema kwamba Emma angeelezea maandiko na kuwafundisha waumini wa Kanisa. Alimwambia Emma amweke Yeye kwanza katika maisha yake na kushika maagano yake. Alimuahidi Emma angekuwa na Roho Wake. Alimtaka ajifunze, akue, na kupokea baraka Zake.

Mafundisho na Maagano 25:2, 6–10, 15.

Emma akiongoza wimbo wa dini katika mkutano wa Kanisa.

Bwana pia alimwambia Emma kwamba Yeye anapenda kuwasikia watoto Wake wakiimba. Alisema nyimbo za Watakatifu Wake ni kama sala Kwake. Alimwomba Emma kutengeneza kitabu cha nyimbo ambazo Watakatifu wangeweza kuimba kutoka humo kwa pamoja. Emma alipata nyimbo nyingi nzuri kuhusu Bwana na injili Yake na kuziweka kwenye kitabu cha nyimbo za dini.

Mafundisho na Maagano 25:11–12; Saints, 1:221–22

Emma na Joseph wakiwapungia mkono majirani.

Maisha ya Emma na Joseph yaliendelea kubadilika, lakini Emma alijua kwamba Bwana alimpenda na alikuwa na lengo kwa ajili yake. Alimtumikia Bwana na watu waliomzunguka. Alisaidia Kanisa la Yesu kukua.

Mafundisho na Maagano 25:13–15; Saints, 1:221–23