“Akina Knight na Wengine Wanakusanyika Sayuni,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)
“Akina Knight na Wengine Wanakusanyika Sayuni,” Hadithi za Mafundisho na Maagano
Desemba 1830–Agosti 1831
Akina Knight na Wengine Wanakusanyika Sayuni
Kutii wito wa Bwana
Polly na Joseph Knight waliishi na familia yao huko New York. Walimjua Nabii Joseph vizuri. Baada ya kujifunza injili, walichagua kujiunga na Kanisa. Wakati Bwana alipowaomba Watakatifu kuhamia Ohio, akina Knight walitii.
Mafundisho na Maagano 37; Saints, 1:33, 94, 109–110
Akina Knight walikuwa na furaha walipowasili Ohio. Leman Copley, muumini wa Kanisa, alisema baadhi ya Watakatifu wangeweza kuishi katika ardhi yake. Kulikuwa na nafasi ya kutosha ya kupanda mazao na kujenga nyumba. Joseph Knight na wanawe walifanya kazi kwa bidii ili kuyaandaa mashamba tayari kwa ajili ya kupanda.
Saints, 1:126–27
Lakini siku moja, Leman alibadilisha mawazo yake kuhusu ardhi yake. Hakutaka Watakatifu kuishi huko tena. Aliwaambia akina Knight na kila mtu mwingine waondoke.
Saints, 1:127
Watakatifu walikuwa na wasi wasi. Sasa hawakuwa na mahali pa kuishi. Walimwuliza Nabii Joseph kile walichopaswa kufanya.
Mafundisho na Maagano 54; Saints, 1:127
Bwana alisema kwamba Watakatifu hawa wanapaswa kwenda Missouri na kujenga Sayuni. Sayuni ingekuwa mji ambapo watu wa Bwana wangeweza kukusanyika. Katika Sayuni, wangejenga hekalu ambapo wangefanya maagano, au ahadi na Mungu. Yeye angewabariki kama wangeshika maagano haya. Akina Knight walikuwa na shauku ya kwenda huko.
Mafundisho na Maagano 29:1–8; 42:30–36; 45:59–66; 54:6–9; 57:1–2; Saints, 1:128
Wakati akina Knight waliposafiri kwenda Missouri, Polly akawa mgonjwa sana. Mume wake, Joseph, na wanawe walihofia kwamba hangeishi kwa muda mrefu zaidi. Lakini Polly aliiambia familia yake kwamba alitaka kuwa Sayuni kabla ya kufariki. Alitaka hivyo zaidi ya kitu kingine cho chote!
Saints, 1:128
Baada ya safari ndefu, Akina Knight waliwasili Missouri. Polly alikuwa na shukrani sana kwa Bwana kwamba alikuwa ameishi kuiona. Akina Knight walidhani nchi ilikuwa nzuri. Walikuwa na imani kwamba wangeweza kutii amri ya Bwana ya kujenga Sayuni huko.
Saints, 1:132
Watakatifu walisema sala maalum na kuiita ardhi hiyo Sayuni, ambapo watu wa Bwana wangekuja. Nabii Joseph aliweka jiwe ili kuweka alama mahali ambapo kona ya hekalu ingekuwa. Siku chache baadaye, Polly alifariki. Bwana aliahidi kwamba Watakatifu walio kuja Sayuni na kufa wangepumzika mbinguni.
Mafundisho na Maagano 59:1–2; Saints, 1:132–33