Hadithi za Maandiko
Elijah Able


“Elijah Able,” Hadithi za Mafundisho na Maagano (2024)

“Elijah Able,” Hadithi za Mafundisho na Maagano

1838

Elijah Able

Misheni ya imani na ujasiri

Elijah Able akimbatiza Eunice Franklin.

Bwana alimwita mtu aliyeitwa Eliya Able kuwa mmisionari. Elijah alimfundisha Eunice na Charles Franklin kuhusu injili ya Yesu Kristo. Aliwaambia kuhusu Kitabu cha Mormoni na kuhusu Nabii Joseph Smith. Eunice na Charles waliamini kile alichofundisha na walitaka kujiunga na Kanisa. Elijah aliwabatiza.

Saints, 1:316

Elijah akiwa na ndoto.

Elijah aliondoka ili kushiriki injili katika mji mwingine. Usiku mmoja, miezi michache baadaye, alikuwa na ndoto kuhusu rafiki yake Eunice. Katika ndoto, Eunice hakuwa na uhakika tena kwamba Kitabu cha Mormoni kilikuwa cha kweli au kwamba Joseph Smith alikuwa nabii. Wakati Elijah alipoamka, alirudi mara moja kumwangalia Eunice.

Mafundisho na Maagano 75:27; Saints, 1:315–16

Elijah akizungumza na Eunice.

Eunice alishangaa kumwona Elijah mlangoni kwake! Ndoto ya Elijah ilikuwa sahihi: Eunice hakuamini katika Kitabu cha Mormoni au Joseph Smith tena.

Saints, 1:317

Elijah akihubiri shuleni.

Elijah alimwomba Eunice aje amsikilize akihubiri shuleni. Aliposikia maneno ya Eliijah, alihisi Roho Mtakatifu tena. Alijua injili ilikuwa ya kweli!

Saints, 1:317

Elijah akizungumza na watu nje ya shule.

Elijah alimuahidi Eunice angerudi katika wiki mbili kuhubiri tena. Lakini baadhi ya watu katika mji huo hawakumtaka arudi tena. Baada ya Elijah kuondoka, walianza kumwambia kila mtu kwamba Elijah alikuwa ameua watu. Walitoa zawadi kwa ye yote atakayempata.

Saints, 1:318

Eunice akibishana na watu mjini.

Eunice alijua kwamba watu walikuwa wanadanganya kuhusu Eliya. Hakuwa amemuua mtu yeyote. Alikuwa mtu mwema na mtumishi wa Mungu. Alijua uongo wao haungemzuia Elijah asije kwenye mji wao kuhubiri. Eunice aliwaambia watu kwamba Elijah angerudi. “Mungu atamlinda,” alisema.

Saints, 1:318

Elijah akirejea shuleni.

Elijah alirudi. Alikuja kwenye shule ile ile ambayo alikuwa amehubiri hapo awali. Ilikuwa imejaa watu waliotaka akamatwe. Elijah alisimama mbele ya umati. Yeye alisema kama walitaka kumkamata, wanapaswa kufanya hivyo sasa, kabla hajaanza kufundisha. Kama sivyo, wanapaswa kumwacha afundishe.

Saints, 1:318

Watu wakifokasi kwa Elijah anapofundisha.

Hakuna aliyeondoka Eliya alisubiri, lakini umati ulikaa kimya. Eliya aliimba wimbo, alisali, na kufundisha injili ya Yesu Kristo. Nguvu za Mungu zilikuwa pamoja naye. Baada ya kumaliza kufundisha, alizungumza na marafiki zake Eunice na Charles na kuendelea na misheni yake kwa amani.

Saints, 1:319