“Nifundishe kuhusu Sala,” Rafiki, Januari 2025, 46–47.
Misingi ya Injili
Nifundishe kuhusu Sala
Sala ni jinsi sisi tunavyozungumza na Baba wa Mbinguni. Tunasali Kwake katika jina la Yesu Kristo.
Tunaweza kumshukuru Baba wa Mbinguni kwa ajili ya baraka Yeye anazotupatia sisi.
Tunaweza kumwomba Yeye vitu tunavyohitaji. Tunaweza pia kuwaombea watu wengine.
Baba wa Mbinguni daima atasikia sala zetu.
Wakati wa Shughuli
Onesha au zungushia duara picha ambazo zinaonesha kitu unachoweza kusali kwa ajili yake. Ni nini kingine unaweza kusali kukihusu?
Vielelezo na Daniela Sosa