2025
Ono la Kwanza
Desemba 2024


“Ono la Kwanza,” Rafiki, Januari 2025, 26–28.

Hadithi za Maandiko

Ono la Kwanza

Unaweza kusoma hadithi hii katika Joseph Smith—Historia ya 1:1–20.

Joseph Smith akimtazama mtu akilihubiria kundi

Wakati Joseph Smith alipokuwa mdogo, makanisa mengi yalifundisha mambo tofauti kuhusu Yesu Kristo. Joseph hakujua ni kanisa gani la kujiunga nalo.

Joseph Smith akisoma Biblia

Siku moja, alisoma Yakoba 1:5 katika Biblia. Ilisema kama tunahitaji hekima, tunaweza kumwomba Mungu. Joseph aliamua kufanya hivyo.

Joseph Smith akitembea msituni

Katika siku nzuri ya majira ya kuchipua, Joseph alikwenda msituni kusali kwa Baba wa Mbinguni.

Joseph Smith akisali

Joseph alipiga magoti na kuanza kusali. Lakini kisha alihisi giza likimzunguka. Joseph aliogopa. Alimwomba Mungu msaada.

Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wakimtokea Joseph Smith

Ghafla, Joseph aliona mwanga mkali ukishuka kutoka mbinguni. Aliwaona Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wamesimama juu angani. Baba wa Mbinguni aliliita jina la Joseph. Kisha Yeye alimwonyesha Yesu na akasema, “Huyu ni Mwanangu Mpendwa. Msikilize Yeye!”

Yesu Kristo

Yesu alimwambia Joseph asijiunge na kanisa lolote.

Joseph Smith akiwa amepiga magoti akitazama juu

Joseph angesaidia kurejesha utimilifu wa injili duniani.

Joseph Smith akitabasamu na kuondoka msituni

Joseph hakukanganyikiwa tena. Alijawa na shangwe! Alijua Mungu alimpenda. Baadhi ya watu hawakuamini kwamba alikuwa amewaona Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo, lakini yeye alijua ilikuwa ni kweli.

PDF ya hadithi