“Miwani Iliyopotea,” Rafiki, Januari 2025, 44–45.
Miwani Iliyopotea
Hadithi ya kweli kutoka Bolivia.
Ilikuwa ni siku ya kwanza shuleni. Andrés alikuwa na furaha sana! Alikuwa darasa la kwanza sasa. Alikuwa mtoto mkubwa!
Lakini alipofika shuleni, shule ilionekana kubwa sana na ya kutisha, hata kwa mtoto mkubwa. Aliushika mkono wa Mama kwa nguvu sana.
Yote yatakuwa SAWA. Mami alitabasamu. “Msalimie kwa mwalimu wako. Kuwa mwema kwa wanadarasa wenzako. Wala usisahau kutunza miwani yako.
Wiki moja iliyopita, Andrés alipata jozi yake ya kwanza ya miwani. Wazazi wake daima walimkumbusha kuitunza.
Mami alipunga mkono wa kwaheri. “Uwe na siku njema!”
Lakini Andrés hakuwa na siku nzuri. Kitu kibaya kilitokea!
Alimkimbilia Mami baada ya shule. “Nimepoteza miwani yangu!” alilia. “Nimeangalia kila mahali, lakini sikuwezai kuipata!”
“Lo Hapana!” Mami alionekana mwenye wasiwasi. “Acha tumwombe Baba wa Mbinguni kwa ajili ya msaada.”
“Unadhani sala itafanya kazi?” aliuliza.
“Acha tujaribu na tuone. Baba wa Mbinguni daima husikia sala zetu,” Mami alisema.
Andrés na Mami walisema sala. Walimwomba Baba wa Mbinguni amsaidie Andrés aipate miwani yake.
Siku iliyofuata shuleni, Andrés alikuwa bado na huzuni. Kisha mvulana akamjia.
“Nadhani hii ni yako.” Mvulana alishikilia jozi ya miwani. “Niliipata kwenye uwanja wa mpira.”
Andrés alichukua miwani. Ilikuwa ni yake. Hakuweza kuamini.
Baada ya shule, alimkimbilia Mami na kumpa kumbatio kubwa.
“Umeipata miwani yako!” alisema. “Utakuwa umepata furaha sana kuwa nayo.”
“Ndio!” Andrés alisema. “Lakini nina furaha zaidi kwa sababu ya kile nilichojifunza.”
“Na hicho ni nini?”
Andrés alitoa tabasamu bashasha. “Sala inafanya kazi!”
Vielelezo na Susanna Teodoro