Imeandikwa na Wewe
Je, Ni Kweli Yesu ni Halisi?
Siku moja nilijiunga na ndugu zangu mezani kujifunza maandiko kifamilia. Mama yangu alianza somo letu la Njoo, Unifuate , lakini sikutoa usikivu wa kweli. Nilikuwa nikifikiria kitu kingine: Je, ni kweli Yesu ni halisi?
Kanisani na katika darasa la Watoto tulijifunza kwamba Yeye kweli ni halisi, lakini mimi mwenyewe sikuwa najua hilo. Niliwaza tena na tena, lakini sikuweza kupata jibu.
Baada ya kujifunza maandiko, nilimuuliza mama yangu, “Je, ni kweli Yesu ni halisi?”
“Swali zuri,” alisema. “Je, unaonaje wewe ukisali kuhusu hilo?”
“SAWA,” nilisema.
Usiku ule nilisali na kuuliza, “Baba wa Mbinguni, ni kweli Mwanao ni halisi?” Kisha nilipata hisia nzuri sana ndani yangu. Nilijua Mungu alikuwa amejibu sala yangu. Baada ya hapo, nilisema sala ya shukrani kwa Baba wa Mbinguni kwa kunijibu. Ninajua Yeye anasikiliza sala zangu na kwamba Yeye pia atasikiliza sala zako.
Kielelezo na Emily Davis