Kujifunza na Kukua
Tulikuja duniani ili tuweze kujifunza na kukua na kuwa kama Baba wa Mbinguni siku moja (ona Musa 1:39). Wakati mwingine tunafanya chaguzi ambazo hatujisikii kujivunia. Tunapotenda dhambi au kufanya kosa, ni nafasi kwa ajili yetu kumgeukia Yesu Kristo.
Unaweza daima kukua na kujaribu tena wakati unapofanya kosa au uchaguzi mbaya. Baba wa Mbinguni na Yesu Kristo wanakupenda kikamilifu na daima wanaweza kukusaidia!
Kila Mmoja Anaweza Kutubu
Kuchagua kufanya kitu unachojua ni kinyume na amri za Mungu ni dhambi. Baba wa Mbinguni alijua sote tungetenda dhambi na kufanya chaguzi mbaya. Hiyo ndiyo sababu Yeye alimtuma Mwanawe, Yesu Kristo. Kwa sababu Yake, tunaweza kutubu, kuhisi upendo Wake, na kufanya chaguzi bora (ona Enoshi 1:5–6). Kumbuka, Bwana ameahidi: “Yule ambaye ametubu dhambi zake, huyu anasamehewa, na Mimi, Bwana, sizikumbuki tena” [Mafundisho na Maagano 58:42].”14
Kujifunza kutokana na Makosa
Makosa ni kitu unachofanya kama ajali. Wakati mwingine makosa yanaweza kukufanya uhisi huzuni au aibu. Lakini hatuhitaji kufokasi kwenye makosa yetu! Tunaweza kujifunza kutokana na hayo na kuachana nayo. Yesu Kristo anaweza kutusaidia kwa hayo pia.
Kielelezo na Tatsiana Burgaud