“Kumfuata Yesu huko Kenya,” Rafiki, Novemba. 2024, 10–11.
Kumfuata Yesu huko Kenya
Kutana na Martin!
Jinsi Martin Anavyomfuata Yesu
Martin anamfuata Yesu kwa kujifunza kumhusu Yeye. Wakati Martin alipokutana na wamisionari, walimpa kijitabu kuhusu Yesu Kristo. Martin ana ulemavu wa kuona, hivyo hakuweza kusoma maneno madogo. Lakini bado alitaka kujifunza zaidi.
Wamisionari walimpa Martin nakala ya Kitabu cha Mormoni kwa breli. Breli ni aina ya lugha iliyoandikwa kwa ajili ya watu ambao ni vipofu au wenye ulemavu wa kuona.
Martin alichagua kubatizwa pamoja na baba yake. “Ninashukuru kwa ajili ya Kanisa la Yesu Kristo,” Martin anasema. “Mimi najua ni la kweli.”
Kuhusu Martin
Umri: miaka 10
Kutoka Nairobi, Kenya
Lugha: Kiingereza, Kiswahili,
Malengo: 1) Kueneza nuru ya Yesu Kristo. 2) Kutumikia misheni. 3) Kuwa mwanasheria.
Mambo ayapendayo : Kucheza chesi, kumsaidia baba yake na biashara yake ya kutengeneza nguo
Familia: Martin, Baba, kaka mkubwa
Mambo Ayapendayo Martin
Hadithi ya Kitabu cha Mormoni: Wakati mizigo ya Wanefi ilipofanywa kuwa miepesi (ona Mosia 24)
Likizo: Siku ya Mashujaa
Matunda: Mapeazi
Rangi: Bluu
Wimbo wa Watoto: “I Am a Child of God” (Kitabu cha Nyimbo za Watoto, 2–3)