“Mwili Wako ni Zawadi!” Rafiki, Mei 2025, 38–39
Mwili Wako ni Zawadi!
Miili huja katika ukubwa, maumbo, uwezo, na rangi tofauti. Kila mwili mmoja ni zawadi ya ajabu kutoka kwa Mungu na sehemu muhimu ya mpango Wake!
Miili yote inastahili heshima. Zungumza kwa ukarimu kuhusu mwili wako mwenyewe na ya wengine. Watu wangeweza kusema mambo yasiyo ya ukarimu kukuhusu wewe, lakini huna haja ya kuyaamini au kufokasi kwenye maneno yao.
Mwili wako ni nyumba ya roho yako. Kile unachokiweka katika mwili wako na ubongo wako ni muhimu! Tunaweza kuitunza miili yetu kwa kula vyakula bora, kufanya mazoezi, na kupata usingizi wa kutosha.
Tunaweza kutunza roho zetu kwa kumsikiliza Roho Mtakatifu, kusali, na kuchagua mema.
Watu wengi wana zaidi ya mifupa 200. Mifupa yako inausaidia na kuulinda mwili wako. Misuli yako inakusaidia kusogea, kutembea, na kukimbia.
Vali katika moyo wako hufunguka na kufunga zaidi ya mara 100,000 kwa siku. Hii husaidia kusukuma damu kupitia mwili wako wote.
Ubongo wako hufanya kazi kwa bidii kuelewa kila kitu unachoona, kusikia, na kuhisi. Ni imara na haraka zaidi kuliko kompyuta yoyote.
Unapokuwa mkubwa, mwili wako utakua. Baba wa Mbinguni aliusanifu mwili wako ili uendelee kubadilika maisha yako yote!
Kile unachofanya na mwili wako ni muhimu zaidi kuliko vile unavyoonekana. Je, unautumia kuwatendea wengine na wewe mwenyewe kwa ukarimu na kumfuata Yesu Kristo?
Usilinganishe mwili wako na wa mtu mwingine yeyote. Kambuka, mwili wako ni zawadi kutoka Baba wa Mbinguni!
Vielelezo na Jeff Harvey