“Kutembea katika Nyayo Zake,” Rafiki, Mei 2025, 17.
Imeandikwa na Wewe
Kutembea katika Nyayo Zake
Siku moja familia yangu ilienda kuteleza na sleji pamoja na bibi na baba yangu. Tulitembea hadi kwenye eneo lililokuwa limefunikwa kwa futi kadhaa za theluji safi. Ilikuwa vigumu sana kutembea ndani! Dada yangu alikuwa na wakati mgumu kutembea katika theluji, hivyo baba yangu alisema, “Tembea tu katika nyayo zangu.”
Mimi na dada yangu tulianza kukanyaga nyayo zake. Baada ya muda nilitaka kujaribu kutembea peke yangu kwa muda kidogo. Nilipotembea peke yangu kwenye theluji, ilikuwa ni vigumu zaidi!
Kutembea katika nyayo za baba yangu ilikuwa rahisi kwa sababu tayari alifanya sehemu ngumu ya kutembea kwenye theluji. Nina ushuhuda kwamba Yesu Kristo tayari alifanya sehemu ngumu zaidi. Kama utatembea katika nyayo za Yesu, maisha yako yatakuwa rahisi pia.
Kielelezo na Abby Rummler