2025
Kopo la Maajabu
Mei 2025


“Kopo la Maajabu,” Rafiki, Mei 2025, 18–20.

Kopo la Maajabu

“Je, tumewahi kuwapa majina watu kama hayo?” Aliuliza Baba.

Hadithi ya kweli kutoka Marekani.

Mvulana na msichana wakiangalia kopo kubwa

“Hii ni nini, Mama?” Sadie alivuta kopo kubwa la bati kutoka nyuma ya kabati. “Halina lebo juu yake.”

“Nilisahau kuhusu hilo,” Mama alisema. “Lebo zilikuwa zimetoka kwenye baadhi ya bidhaa za makopo, hivyo duka lilikuwa linaziuza kwa bei nafuu. Nilinunua moja. Niligundua yawezekana ilikuwa ni makopo ya kunde.”

Sadie alikunja uso. Kunde za makopo hazikuwa za kupendeza kwake.

Mama alichukua kopo na kuligeuza. “Zitaharibika hivi karibuni. Ni vyema tuzile leo.” Aliweka kopo kwenye meza.

“Hiyo ni nini?” Kaka mkubwa wa Sadie, Jason, aliuliza.

“Nani anayejua?” Sadie alisema. “Mama anafikiri ni kunde.”

Jason alitingisha kopo. “Haisikiki kama kunde. Nadhani ni maharage.”

Hiyo ilimpa Sadie wazo. Alichukua mkanda na kalamu ya kuwekea alama na kuandika “kunde” kwenye kipande kimoja cha karatasi na “maharage” kwenye kingine. Alivibandika kwenye kopo.

Kisha alifikiria kwa dakika moja na kuandika “mchuzi wa nyanya” kwenye kipande kingine.

Kisha Baba akaingia jikoni. “Nini kinaendelea?”

“Tunacheza mchezo,” Mama alisema. “Bahatisha kilichopo kwenye kopo.”

Kitufe cha mawazo chenye makopo matatu na lebo tofauti

Baba aliinua kopo, akalitingisha kwa nguvu, na kulinusa. “Uyoga!” alitangaza.

Kila mtu aliguna. “Sio uyoga!” Sadie alisema. Hiyo ilikuwa mbaya zaidi kuliko kunde, maharage, na mchuzi wa nyanya. “Labda tunapaswa kutupa tu kopo hili.”

“Je, hamna dukuduku kujua nini hasa kipo ndani?” aliuliza Mama.

Baba alichukua kifungua kopo. “Mimi nataka kujua!”

Wakati Baba akifungua kopo, Sadie alifunika macho yake. Lakini alipovuta kifuniko, Sadie alishangaa. Kopo lilikuwa limejaa tunda tamu.

“Tamuu!” alisema alipokuwa akiangalia pea zilizokatwa, zabibu, cheri, na pichi.

Kopo lililobinuliwa na msichana anayetabasamu akiwa ameshikilia bakuli

Jason alileta mabakuli na vijiko. “Acha tule!”

Sadie aliweka baadhi ya matunda kutoka kwenye kopo ndani ya bakuli lake. “Siwezi kuamini sote tulikuwa tumekosea,” alisema. “Nilikuwa na uhakika kulikuwa na kitu kilicho kitamu ndani.”

“Je, tumewahi kuwapachika majina watu kama hivyo?” aliuliza Mama.

“Unamaanisha nini?” Sadie aliuliza.

Baba aliweka bakuli lake mezani. “Tunaamua vile walivyo ndani, wakati yote tunayoweza kuona ni ya nje.”

Sadie aliwaza kuhusu hilo. “Wakati Samara alipokuwa mpya shuleni, nilidhani hakuwa rafiki. Lakini nilijifunza kwamba hakuweza tu kuongea lugha yetu vizuri sana. Sasa tunacheza wakati wote!”

Wasichana wawili wakicheza na mpira pamoja

“Huo ni mfano mzuri,” mama alisema.

“Wakati mwingine ninahisi kubandikwa lebo, Jason alisema kwa upole. “Watoto shuleni wanasema ninapata alama nzuri kwa sababu tu mwalimu ananipenda. Lakini ukweli ni kwamba, ninafanya kazi kwa bidii na kufanya kazi zangu zote za nyumbani.”

“Lebo zinaweza kuumiza, sivyo?” alisema Baba.

Jason aliitikia kwa kichwa.

Sadie alimaliza kuuma tunda lake la mwisho. “Lakini je, lebo zote ni mbaya? Kwenye duka unahitaji kujua unanunua nini hasa.”

“Uko sahihi,” Baba alisema. “Kwa hiyo ni wakati gani lebo ni nzuri?”

Jason alinyanyua kijiko chake. “Wakati zinapokuwa za kweli!”

“Na nani anajua nini hasa kipo ndani ya mtu?” aliuliza Mama.

“Baba wa Mbinguni,” Sadie na Jason walisema pamoja.

“Nimeielewa hiyo.” Sadie alisema. “Mimi mtoto wa Mungu. Hiyo ndiyo lebo sahihi kwangu.”

“Na mimi,” Jason alisema.

“Na mimi!” alisema Baba.

“Kwa kila mtu.” Mama alitabasamu. “Kwa hivyo hatupaswi kuwapachika lebo watu kulingana na kile tunachokiona kwa nje, au kuamini lebo za uongo tulizopewa. Kwa kuwa Mungu pekee anajua vile tulivyo hasa ndani yetu.”

Sadie aliandika kwenye kipande kipya cha mkanda na kukibandika kwenye fulana yake. “Mtoto wa Mungu,” alisema. Sadie alitabasamu. Alipenda lebo hiyo vyema zaidi ya zote.

PDF ya hadithi

Vielelezo na Róisín Hahessy