“Halo kutoka Malaysia!” Rafiki, Mei 2025, 12–13
Halo kutoka Malaysia!
Jifunze kuhusu watoto wa Baba wa Mbinguni ulimwenguni kote.
Malaysia ni nchi iliyopo Kusini Mashariki mwa Asia. Angalau watu milioni 33 wanaishi huko. Zaidi ya lugha 130 huzungumzwa huko, ikijumuisha Kimalayi na Kiingereza.
Duara Kubwa Zaidi Duniani la Barabarani
Duara moja la barabarani huko Putrajaya, Malaysia, ni maili 2.1 (kilomita 3.4) kwa upana. Ni duara kubwa zaidi la barabarani ulimwenguni!
Misitu ya Kale ya Mvua
Taman Negara ni mojawapo ya misitu mikuu ya mvua duniani. Ina angalau umri wa miaka milioni 130!
Minara Miwili
Petronas Towers ni ghorofa mbili ndefu ambazo zina ghorofa 88 kwa urefu. Nusu ya urefu kuna daraja la angani la kutembea kati ya majengo.
Wanyama wenyeji
Kuna wanyama wengi wa kipekee nchini Malaysia! Baadhi ya wanyama ni dubu wa jua, orangutani, na tapirsi.
Pango Kubwa
Sarawak Chamber huko Malaysia ni kubwa sana kiasi cha kuweza kutosheleza ndege nane za jumbo kwa pamoja! Pango lina urefu wa futi 2,300 (mita 700) na upana wa futi 980 (mita 300).
Vielelezo na Josh Talbot