2025
Kwa Ajili ya Watoto Wakubwa
Mei 2025


“Kwa Ajili ya Watoto Wakubwa,” Rafiki, Mi 2025, 34–35.

Kwa Ajili ya Watoto Wakubwa

Maneno kutoka Kwako

Kwa kawaida ninahisi woga kidogo ninapokwenda kulala. Ninaposali, ninahisi amani na kusinzia haraka.

Vance R., miaka 9, Utah, Marekani

Nilipoteza kitabu changu cha shule na kusali kwa Baba wa Mbinguni anisaidie. Nilikuta kimefichika chini ya nguo zangu mbele yangu. Ilinisaidia kuelewa jinsi sala ilivyo muhimu.

Minh P., umri miaka 11, Mkoa wa Hanoi, Vietnam

Mchungaji Mwema

Jifunze jinsi ya kumchora mchungaji na kondoo wake. Ni kwa jinsi gani Yesu Kristo hutusaidia wakati tunapohisi kama kondoo aliyepotea?

Kusimama Mahali Patakatifu

Yesu Kristo anatutaka sisi “tusimame mahali patakatifu” (Mafundisho na Maagano 45:32). Tunaweza kumhisi Roho katika mahali patakatifu. Fuata njia ya kila mtoto ili kuona mahali patakatifu wanapoenda.

Taa Ndogo

Joseph Smith alifundisha, “Kile Kilicho cha Mungu ni Nuru” (Mafundisho na Maagano 50:24) Wekea duara kitu katika kila safu ambacho hakihusiki hapo!

Ukurasa wa PDF ukiwa na shughuli na nukuu kwa ajili ya vijana wadogo

Vielelezo na Katy Dockrill